Tangazo

February 2, 2015

Airtel yafanya kufuru, Wateja wake kushinda gari Moja Kila Siku


Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel, Beatrice Singano Mallya akizungumza na waandishi wa habari kabla ya kuzindua promosheni kabambe ijulikanayo kama Airtel Yatosha Zaidi katika viwanja vya Mlimani City jijini Dar es Salaam leo Feb. 02.2015. Kushoto ni Mkurugenzi wa Masoko ya Airtel, Levi Nyakundi.PICHA ZOTE/JOHN BADI

Mkurugenzi wa Masoko ya Airtel, Levi Nyakundi (kushoto), na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel, Beatrice Singano Mallya wakifungua kitambaa kuzindua rasmi promosheni hiyo.

Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel, Beatrice Singano Mallya (kushoto) na Mkurugenzi wa Masoko ya Airtel, Levi Nyakundi wakikagua baadhi ya magari yatakayoshindaniwa katika promosheni hiyo. 
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx
·  Kupitia huduma ya Airtel Yatosha
 
·  Promosheni ya Airtel yatosha zaidi itawawezesha wateja wa
Airtel kushinda Toyota IST moja Kila siku


Airtel Tanzania leo imezindua promosheni  kabambe ijulikanayo kama Airtel Yatosha Zaidi kwa wateja wanaotumia vifurushi vya Airtel Yatosha kuweza kujishindia gari Aina ya Toyota IST kila siku.


Akiongea wakati wa uzinduzi wa promosheni hiyo Mkurugenzi wa Masoko ya Airtel Bwana Levi Nyakundi alisema” promosheni hii ni nafasi ya peeke wa wateja wetu wanaojiunga na vifurshi vya Airtel yatosha vya siku, wiki na mwezi kupata faida zaidi kutokana pesa wanazozitumia. Nia yetu kuhakikisha tunatoa huduma na bidhaa bora kwa kupitia huduma yetu ya Airtel Yatosha huku tukiwazawadia wateja wetu zawadi nono.


Tunaamini promosheni hii itawapatia wateja wetu uzoefu tofauti wakati wote wakitumia huduma zetu za Airtel Yatosha. Zaidi ya wateja wetu kijishindia magari promosheni hii ya Airtel Yatosha Zaidi itawapatia wateja wetu vifurushi zaidi “Aliongeza Nyakundi.


Akiongea kuhusu namna ya kushiriki Mkurugenzi wa mawasiliano wa Airtel, Bi. Beatrice Singano Mallya alisema” ili kushiriki kwenye promosheni hii wateja wanatakiwa kuendelea kununua vifurushi vyao vya Yatosha vya siku, wiki na mwenzi.  hakuna gharama ya ziada, kwa kununua vifurushi vya yatosha tayari utakuwa umeunganishwa kwenye droo ya yatosha zaidi na kupata nafasi ya kujishinidia Toyota IST moja kila siku.


Hii ni promosheni ya aina yake ambapo wateja wetu wanazawadiwa kutokana na matumizi yao ya kawaida ya vifurushi vya Yatosha.  Tunatoa wito kwa wale ambao hawajajiunga na vifurushi vya Airtel yatosha kufanya hivi na kupata nafasi ya kushinda gari moja kila siku”, aliongeza  Mallya.


Kununua vifurushi vya yatosha wateja wanaweza au  kupiga *149*99#, kunua kwa kupitia huduma ya Airtel Money au kwa kununua vocha ya Airtel yatosha inayopatikana katika maduka yetu nchi nzima.

Mwaka Jana Airtel ilizindua huduma ya kisasa ya kibunifu na yenye vifurushi vya gharama nafuu sokoni. Kuzinduliwa kwa promosheni hii ya Airtel yatosha Zaidi ni mwendelezo wa dhamira ya Airtel ya kutoa huduma bora huku ikiwazawadia wateja wake kwa kutumia huduma zake.

No comments: