Tangazo

August 31, 2015

UN YAFANYA USAFI SOKO LA TEMEKE STEREO KUADHIMISHA MIAKA 70

IMG_5298
Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy akizungumza machache kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Sophia Mjema (katikati) kabla ya kuanza zoezi la usafi katika soko la Temeke Stereo ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 70 ya Umoja wa Mataifa. Kushoto ni Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez.(Picha zote na Zainul Mzige wa Modewjiblog)
Na Mwandishi wetu
KATIKA kuadhimisho miaka 70 tangu kuanzishwa kwa Umoja wa Mataifa (UN) wafanyakazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini Tanzania na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirkiano wa Kimataifa walijumuika na wakazi wa Temeke katika kufanya usafi kwenye soko la Temeke Stereo.
Shughuli hiyo wameifanya baada ya wiki iliyopita kufanya shughuli za upandaji miti katika miteremko ya mlima Kilimanjaro. Wakiwa katika miteremko ya milima Kilimanjaro walipanda miti 2,000.
Shughuli hizo za kufanya usafi ambazo ziliongozwa na Mratibu wa mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez, zilifanyika katika juhudi za kuleta uhalisia wa utunzaji wa mazingira kama umoja huo unavyofanya.
Akizungumza katika shughuli hizo Mkuu wa wilaya ya Temeke, Sophia Mjema, ambaye alimwakilisha Mkuu wa Mkoa aliupongeza Umoja wa Mataifa kwa kusherehekea miaka 70.
“Nachukua nafasi hii kupongeza watu wa Umoja wa Mataifa nchini Tanzania kwa kufanya shughuli mbalimbali kuelekea maadhimisho ya miaka 70 kwa kupanda miti 2,070 kwenye miteremko ya Mlima Kilimanjaro na hili tendo la leo la usafi kama mwendelezo wa kaulimbiu inayohimiza utunzaji wa mazingira ya“ Sayari moja, watu bilioni 7: Ulinzi wa mazingira ni wajibu wetu,” alisema.
Akisisitiza umuhimu wa kutunza mazingira na usafi, Mkuu huyo wa wilaya alisema wajibu wa kutunza mazingira ni wa kila mtu.
IMG_5365
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez akitoa salamu za Umoja wa Mataifa katika kuadhimisha miaka 70 ya Umoja wa Mataifa ikiwemo kushiriki shughuli mbalimbali za kijamii kwa wananchi na wafanyabiashara wa soko la Temeke Stereo mwishoni mwa juma. Kushoto ni Kaimu Mwakilishi Mkazi wa FAO nchini, Patric Otto. Wa tatu kulia ni mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya Temeke, Sophia Mjema, Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy (wa pili kulia) na Mkuu wa Idara ya Usafi na Mazingira manispaa ya Temeke, Ally Hatibu.

“Kutunza mazingira si wajibu wa mtu mmoja. Ni wajibu wako kama ilivyo kwa jirani yako. Kunapokuwepo na watu wengi mara nyingi hutokea watu ambao hawajali wala kuona umuhimu wa kutunza mazingira, umuhimu wa kufanya haya.

“ Nawaomba wote mlioshiriki katika shughuli hii leo kuwa watu wa kuchunga mazingira katika maeneo yenu mnayofanyia kazi na majumbani kwenu.Hakikisheni mnafundishana na majirani zako katika suala hili na kuhakikisha kwamba kila mmoja anayekuzunguka anawajibika katika kutunza mazingira.”

Akisisitiza menejimenti ya mazingira, Rodriguez, alizungumza kwamba mabadiliko ya tabia nchi na mazingira endelevu ndio ajenda kuu katika malengo endelevu ya maendeleo (SDG’s).
“Mwaka huu jumuiya ya kimataifa itakubaliana kuhusu SDGs na kukamilishwa kwa malengo ya milenia (MDGs). Malengo ya milenia yamewezesha kupatikana kwa mabadiliko makubwa katika kukabiliana na umaskini, afya bora na kiwango kikubwa cha watu wanaojiunga na shule. Mataifa ya Umoja wa Mataifa kwa kupendezwa na mafanikio ya MDGs sasa wanataka kukubaliana kuhusu SDGs.

“ SDG itakuwa na vipengele 17 kikiwamo cha mabadiliko ya tabia nchi. Umoja wa Mataifa umechagua suala la mabadiliko ya tabia nchi kuwa ndio kipaumbele cha mwanzo kwani imebaini kwamba ni tishio kwa maendeleo endelevu. Hii inatokana na ukweli kuwa mabadiliko ya tabia nchi ni ya kweli na ni vyema kila mtu kuwajibika ili kuhakikisha mazingira yetu yanaendelea kuwa mazuri-tukianzia na mazingira yetu yanayotuzunguka” alisisitiza.
Rodriguez alizitaka jamii mbalimbali kutoa kiipaumbele katika kusafisha mazingira na usafi binafsi hasa kipindi hiki ambapo kumezuka ugonjwa wa Kipindupindu kwa mikoa ya Dar es salaam na Morogoro.

“Usafi wa soko hili ni muhimu kwa ajili ya afya yako na uhai mrefu. Afya njema inatuwezesha kuendelea kufanya shughuli zetu mbalimbali za kuchangia ukuaji wa uchumi.Hebu angalia pembeni mwako imetuchukua saa chache kusafisha soko la Temeke na je hamuoni tofauti? Nawaomba wakazi wa Temeke na wafanyakazi wa soko hili kufanya shughuli hizi kila siku kwani maisha yao, afya yao na uchumi unategemea soko hili.”

Pia aliwaalika wananchi wote katika sherehe za miaka 70 za Umoja wa Mataifa zitakazofanyika viwanja vya Mnazi Mmoja Oktoba 13 ili kushiriki kikamilifu katika kuadhimisha siku hiyo ya Umoja wa Mataifa.

Pia alihimiza serikali kuendelea kuelimisha wananchi juu ya utunzaji wa mazingira na athari za mabadiliko ya tabia nchi.
IMG_5475
Mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya Temeke, Sophia Mjema akitoa nasaha zake kwa wananchi na wafanyabiashara wa soko la Temeke Stereo, ambapo aliwataka kuzingatia usafi wa maeneo yao ya biashara pamoja na majumbani ili kuepeukana na mlipuko wa Kipundupindu.

Katika hafla hiyo ya kusafisha soko la Temeke, Umoja wa Mataifa na serikali ya Tanzania kwa pamoja walitoa vifaa vya kufanyia usafi vyenye thamani ya shilingi milioni 10. Vifaa hivyo vilikabidhiwa kwa menejimenti ya soko la Temeke.

Watu wengine walioshiriki katika shughuli hiyo ni pamoja na Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy; mkuu wa wilaya ya Temeke Mheshimiwa Sophia Mjema, akimwakilisha Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam na maofisa wengine wa serikali na wakazi wa Temeke.

Balozi Mushy katika risala yake ya kumkaribisha mgeni rasmi kufanya usafi aliitaka jamii kutambua kwamba usafi ni jukumu la kila mmoja wetu kwani bila usafi madhara yake ni makubwa ikiwamo ya kutunzwa kwa mazingira.

Alilitaka jiji la Dare s salaam ambalo linalinganishwa na majiji mengine duniani kama Nairobi, Kenya; Pretoria Afrika Kusini, Washinton DC na Paris kujifunza kuwa wasafi kwani hata mlipuko wa sasa wa Kipindupindu ni dalili tosha ya kukosekana kwa usafi.

Aidha alisema kwamba suala la usafi si lazima kwenda kujifunza nje kwani ipo miji na mikoa misafi ambayo inaweza kuulizwa wamefanikishaje jambo hilo. Aliitaja miji hiyo ni Moshi, Iringa na Mwanza.

Alisema katika kuadhimisha miaka 70 ya Umoja wa Mataifa, wameamua kufanya usafi wa mazingira katika soko la Temeke kuonesha kwamba inawezekana kufanya usafi kwa kuwajibika kwa lengo la kufanya mazingira yawe masafi na ya uhakika.

Kwa kutekeleza usafi kwa maana nyingine kutasaidia kuondoa gharama zinazoambatana na uchafu wa mazingira.

Alitaka kila mmoja katika soko hilo kuanzia wakulima hadi wachuuzi kuwajibika kwa usafi ili mazingira yawe salama.
IMG_5301
Pichani juu na chini ni wafanyabiashara wa Soko la Temeke Stereo, wananchi na wafanyakazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na wa Wziara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakifuatilia kwa umakini hotuba ya mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Temeke (hayupo pichani).
IMG_5471
IMG_5299
IMG_5285
IMG_5554
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez (katikati) akikambidhi Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Sophia Mjema (kushoto) vifaa vya kufanyia usafi katika Soko la Temeke Stereo ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 70 ya Umoja wa Mataifa. Anayeshuhudia tukio hilo kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy.
IMG_5558
Mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Sophia Mjema akivaa 'gloves' tayari kushiriki zoezi la usafi katika soko la Temeke Stereo ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 70 ya Umoja wa Mataifa.
IMG_5569
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez (kushoto), Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Sophia Mjema pamoja na Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy wakifanya usafi katika maeneo ya wafanyabiashara katika soko la Temeke Stereo.
IMG_5575
Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy akibeba taka katika soko la Temeke Stereo.
IMG_5604
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez na Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Sophia Mjema wakishiriki zoezi la usafi katika soko la Temeke Stereo ikiwa ni sehemu ya kusheherekea maadhimisho ya miaka 70 ya Umoja wa Mataifa.
IMG_5649
Wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa wakijumuika na Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Sophia Mjema pamoja na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa, Alvaro Rodriguez wakiendelea na zoezi la usafi.
IMG_5643
IMG_5633
IMG_5787
Kaimu Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP), Titus Osundina (kulia), Beatrice Mkiramweni pamoja na Jacqueline Namfua wakifanya usafi kwenye maeneo ya soko la Temeke Stereo.
IMG_5789
Kaimu Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP), Titus Osundina akishiriki zoezi la kuzoa taka katika soko la Temeke Stereo.
IMG_5801
IMG_5678
Umoja ni Nguvu: Wafanyabiashara wa soko la Temeke Stereo, wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa na Wizara ya Mambo ya Nje wakishirikiana kwa pamoja kufanya usafi katika soko hilo ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 70 ya Umoja wa Mataifa.
IMG_5695
Petra Karamagi na Nasser Ngenzi wa Shirika la Umoja wa Mataifa wakishikishiriki zoezi la usafi katika soko la Temeke Stereo.
IMG_5704
Afisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano alipomulikwa na kamera ya Modewjiblog
IMG_5683
IMG_5716
Zoezi likiendelea.
IMG_5721
Zoe Glorious katika ubora wake.
IMG_5723
#HapaKaziTu ......Usia Nkhoma Ledama akiwajibika katika zoezi la usafi soko la Temeke Stereo.
IMG_5726
Wafanyakazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na wafanyabiashara wakishirikiana katika zoezi hilo.
IMG_5741
IMG_5756
IMG_5290
Mtaalam wa Mahusiano na Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania, Hoyce Temu (kulia) akiteta jambo na na baadhi ya maafisa wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa walioshiriki kwenye zoezi la kufanya usafi wa mazingira katika soko la Temeke Stereo.

No comments: