Meneja biashara wa kitengo cha Airtel
Money, Bw. Asupya Naligingwa(kushoto) akiongea na waandishi wa
habari wakati wa kutangaza Airtel kugawa gawio la faida la zaidi
ya shilingi billion 5 kwa wateja na mawakala wake wanaotumia
huduma ya Airtel Money nchi nzima. Kushoto ni Afisa Uhusiano wa Airtel Tanzania, Bi. Jane Matinde.
XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX
Dar es
Salaam
Kampuni ya
simu za mkononi ya Airtel leo imetangaza kugawa zaidi ya shilingi
bilioni 5 kwa wateja na mawakala wake wanaotumia huduma ya Airtel Money
nchi nzima.
Uamuzi
huo wa kutoa gawio la faida lililopo katika akaunti ya udhamini ya
wateja wa Airtel Money (Trust account) litawawezesha wateja wa
Airtel kulipwa kiwango kizuri cha gawio la faida. Kiwango hiki cha
pesa kitalipwa kutokana na kiasi cha pesa mteja alichokuwa nacho
kwenye akaunti yake ya Airtel Money kila mwisho wa siku kuanzia March
2014 hadi April 2015.
Akiongea
na waandishi wa habari,Meneja wa kitengo cha Airtel Money, Asupya
Nalingigwa, alisema wanayo furaha kutangaza mgawanyo huu wa gawio
la faida kwa wateja wao baada ya benki kuu ya Tanzania. Kuidhinisha
kutoa pesa hizi katika akaunti ya udhamini ya pesa za
wateja wa
Airtel Money ijulikanayo kama trust account.
Aliongeza
kwa kusema wateja wa Airtel Money watapata sehemu ya gawio lao
kulingana na salio wanalokuwa nalo kwenye akaunti zao kila siku.
"Tunaamini
kiasi hiki cha pesa kitachangia kwa kiasi kikubwa katika kuboresha
maisha ya watanzania wengi , kuwahamasisha wateja wasiofikiwa na huduma
za kibenki kutumia mfumowa pesa kwa njia ya simu. Vilevile wateja wetu
wa Airtel Money wataendelea kutumia huduma za pesa kupitia simu za
mkononi, kufanya miamala yao ya kila siku na kutunza pesa zao ili kupata
gawio lao kila watakapo weka pesa katika akaunti zao za Airtel
Money". Aliongeza Nalingigwa
Uamuzi
huu wa kutoa gawio la faida kwa wateja ni wakuungwa mkono kwani unachochea
na kuboresha matumizi ya huduma za kifedha kupitia simu za mkononi ,
ukizingatia takribani asilimia 85% ya watanzania bado hawajafikia na
huduma za kibenki.
Airtel
imekuwa mstari wa mbele katika kutoa huduma za kibunifu za kifedha
kupitia simu za mkononi ikwemo NFC huduma inayokuwezesha kufanya malipo
kupitia kadi, Mikopo ya Timiza na huduma nyingine nyingi.
Katika
maelezo yake Naligingwa aliahidi Airtel kuendelea na dhamira yake
ya kuzindua huduma bora na za kisasa katika mienzi ijayo ili kuwanufaisha
watanzania waishio maeneo ya mijini na vijijini
About
Bharti Airtel
Bharti
Airtel Limited is a leading global telecommunications company with
operations in 20 countries across Asia and Africa. Headquartered in New
Delhi, India, the company ranks amongst the top 3 mobile service
providers globally in terms of subscribers. In India, the company's
product offerings include 2G, 3G and 4G wireless services, mobile
commerce, fixed line services, high speed DSL broadband, IPTV, DTH,
enterprise services including national & international long distance
services to carriers. In the rest of the geographies, it offers 2G, 3G
and 4G wireless services and mobile commerce. Bharti Airtel had over 335
million customers across its operations at the end of August 2015. To
know more please visit, www.airtel.com<http://www.airtel.com>
No comments:
Post a Comment