Tangazo

October 22, 2015

Ziara ya Mama Mwanamwema Shein Mkoa wa Kaskazini Unguja

Muasisi wa Umoja wa Wanawake Zanzibar Mama Fatma Karume akisalimiana na Viongozi wa Umoja wa Wanawake Tanzania UWT alipowasili katika viwanja vya ukumbi wa mkutano wa jengo la Wakorea Kibokwa Wilaya ya Kaskazini A Unguja kuhudhurika mkutano wa Mama Mwanamwema Shein na Viongozi hau wa UWT.
Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein, akisalimiana na Viongozi wa UWT Wilaya ya Kaskazini A Unguja.kwa ajili ya kuzungumza na Wanawake hao kuwaombea Kura Wagombea wa CCM. 
Naibu Katibu Mkuu wa UWT Zanzibar Salama About Talib, akizungumza na Viongozi wa UWT Wilaya ya Kaskazini A Unguja na kuwakaribisha Viongozi kuzungumza na Wanawake hao.
Makamu Mwenyekiti Mstaaf wa UWT Zanzibar Balozi Amina Salum Ali, akizungumza na Viongozi wa UWT wa Wilaya ya Kaskazini A Unguja na kuwataka kukipigia Kura Chama cha Mapinduzi kwa maendeleo na kudumisha amani Zanzibar kupitia Mgombea wake wa Urais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein,
Kada wa CCM Bi Asha Abdalla Juma akiwasalimia Viongozi wa Umoja wa Wawanawakev Tanzania Wilaya ya Kaskazini A Unguja na kuwaomba kura kuwapigia Wagombea Ubunge Uwakilishi na Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein na Mgombea Urais Tanzania Dk John Pombe Magufuli. 

Mke wa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mama Asha Balozi Seif akitowa nasaha zake kwa Viongozi wa Wanawake wa Wilaya ya Kaskazini A Unguja kutumia nafasi yao kuipigia kura CCM 
Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein, akiwahutubia Viongozi wa Umoja wa Wanawake wa UWT wa Wilaya ya Kaskazini A Unguja wakati wa ziara yake ya kuwaombea Kura Wagombea wa CCM. mkutano huo umefanyika katika ukumbi wa Mkorea Kibokwa Wilaya Kaskazini A Unguja. 
Viongozi wa UWT Wilaya ya Kaskazini Unguja wakimsikiliza Mama Mwanamwema Shein akitowa nasaha zake kwa Wanawake hao wakati wa mkutano wake wa kuwaombea kura Wagombea wa CCM
Viongozi wa Wanawake wa Wilaya ya Kaskazini A Unguja wakimsikiliza Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein, akitowa nasaha zake wakati wa mkutano wake wa kuwaombea Kura Wagombea CCM na Mgombea Urais wa Zanzibar Ali Mohamed Shein na Mgombea Urais wa Tanzania Dk John Pombe Magufuli ulioganyika katika ukumbi wa Wakorea Kibokwa Zanzibar. 
Imetayarishwa na OthmanMapara.Blogspot Zanzinews.com Email.othmanmaulid@gmail.com Phone 0777424152 or 0715424152

No comments: