Tangazo

January 13, 2016

Waziri Mavunde azindua Msimu wa Pili wa Airtel ‘Fursa Tunakuwezesha’

Naibu Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Bunge, Sera, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu), Anthony Mavunde ( wa pili kushoto), Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel, Sunil Colaso (wa pili kulia) na Mshauri wa Mradi wa Airtel Fursa Tunakuwezesha, Mhandisi George Mulamula wakizindua msimu wa pili wa mradi huo, jijini Dar es Salaam Januari 11.2016. Kushoto ni Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel, Beatrice Singano. PICHA ZOTE/JOHN BADI WA DAILY MITIKASI BLOG
Naibu Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Bunge, Sera, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu), Anthony Mavunde akizungumza wakati wa uzinduzi wa msimu wa pili wa Mradi wa Airtel Fursa Tunakuwezesha.  
Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel, Sunil Colaso akizungumza wakati wa uzinduzi huo.
Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel, Beatrice Singano akizungumza wakati wa uzinduzi huo.
Meneja wa Huduma za Jamii wa Airtel, Hawa Bayumi akizungumza wakati wa uzinduzi huo.
Mmoja wa vijana wajasiriamali walionufaika na msimu wa kwanza wa Mradi huo, akitoa ushuhuda wakati wa uzinduzi huo.

XXXXXXXXXXXXXXXXX


* Zaidi ya shilingi billion 1 kusaidia  miradi ya kuwawezehsha vijana 

Dar es Salaam

 KAMPUNI ya simu ya mkononi ya Airtel leo imezindua msimu wa pili wa mradi wake wa kuwawezesha vijana ujulikanao kama "Airtel FURSA" kwa lengo kuendelea kudhihirisha kutimiza dhamira yake kuendeleza huduma za kijamii nchini Mradi wa "Airtel FURSA" ulizinduliwa Mei 2015, ukiwa na lengo la kuwawezesha vijana kwa kuwapatia mbinu mbalimbali za biashara na vifaa vitakavyowawezesha kukuza biashara zao.

Msimu wa kwanza wa "Airtel FURSA"  umewawezesha vijana zaidi ya 2500
wenye umri kati ya miaka 18 hadi 24 kupata mafunzo ya biashara na wengine 13 wafanyabiashara chipukizi wanaofanya vizuri zaidi kupokea
vifaa vilikvyowasaidi kuboresha biashara zao na kutengeneza fursa zaidi kwa jamii inayowazunguka.

Akiongea wakati wa uzinduzi, Mkurugenzi mkuu wa Airtel Bw, Sunil Colaso, alisisistiza dhamira ya kampuni yake  kuwawezesha vijana na kutambua mchango walio nao katika kuendesha uchumi wa Tanzania
" Mradi huu wa "Airtel FURSA"  unadhihirisha dhamira yetu ya kuwawezesha vijana wa kitanzania wenye malengo ya kuinua maisha yao na kutimiza ndoto zao. Msimu wa kwanza wa "Airtel FURSA" umetoa matokeo mazuri sana na  tumefanikiwa  kugusa maisha ya  maelfu ya vijana wengi kutoka katika mikoa mbalimbali nchini,"

"Katika msimu huu wa pili tunawekeza takribani  shilingi  billion moja ili  kuweza kufikia vijana wengi zaidi ambao wako tayari kutumia fursa na vipaji vyao. Tutaendelea kuwapatia mafunzo ya kibiashara, misaada ya vifaa na kuanzisha mfumo wakisasa wa mafunzo kupitia simu zao za mkononi" alisema Colaso

Akizindua rasmi mradi wa "Airtel FURSA" Naibu waziri  Wizara ya Kazi Vijana na Ajira Anthony Mavunde aliwapongeza Airtel kwa kuanzisha  na kuwekeza kwenye mradi huu mkubwa na kutoa wito kwa vijana kutumia fursa hii ili kuboresha maisha yao. alisema Mh Mavunde.

"Nchi yetu ya Tanzania imebarikiwa kwa kuwa na rasilimali, zikiunganishwa pamoja na fulsa zinazoletwa na miradi kama hii ya "Airtel FURSA" ni wazi vijana wenye malengo Dhahiri ya kujiendeleza wataweza kuboresha maisha yao. Napenda kuwahasa vijana wetu kutumia fursa hii na kufanya kazi kwa bidii:"

"Serikali chini ya Wizara yetu na itaendelea kushirikia Airtel na kufanya kazi kwa pamoja huku ikiweka mazingira bora yatakayochochea vijeza ana kupata fursa ili waweze kuchangia katika kuendeleza  uchumi wa nchi" aliongeza Mavunde.


"Airtel FURSA"  ni mradi endelevu unaowalenga vijana nchi nzima kwa kuwapatia vifaa  ,mafunzo ya biashara na mafunzo mbalimbali kupitia mtandao ili kufikia malengo yao. Kutuma maombi tuma ujumbe mfupi
kwenda namba 15626 ikiwa na taarifa zifatazo Jina, umri, aina ya biashara unayoifanya, mahali na namba za simu. Unaweza pia kutuma maombi yako kwa kupitia barua pepe ya
airtelfursa@tz.airtel.comairtelfursa@tz.airtel.com>. Or tembelea tovuti yetu ya www.airtel.com<http://www.airtel.com>  na ujaze fomu yako ya maombi.

No comments: