·
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx
- Wanafunzi wa IT wa
chuo IFM wahimizwa kushirikiana na Airtel
Wanachuo kutoka chuo cha usimamizi wa fedha (IFM) kitengo cha IT,
wamefanya ziara ya mafunzo kwenye duka la kisasa la Airtel Expo lililopo katika
ofisi kuu za Airtel mtaa wa morroco Dar es salam ikiwa ni mwendelezo wa kutanua
wigo wa kutoa huduma zenye ubora za kibunifu kwa wateja wake.
Wanachuo hao waliweza kujifunza mambo mengi juu ya kampuni hiyo
inavyofanya kazi kuanzia huduma zake hadi bidhaa zinazouzwa na kampuni hiyo.
Ikiwemo Modem iliyozinduliwa hivi karibuni maarufu kama modem ya maajabu
Wingle Modem inayouweza kutumika na zaidi ya watu 10 kwa wakati mmoja,
Simu za Kisasa za gharama nafuu na zenye OFA nzuri
Wanafunzi hao pia wamejionea jinsi duka la Airtel Expo
linavyohudumia wateja wengi kwa kutumia teknolojia ya hali ya juu ya
kidigitali.
Mkurugenzi wa Airtel huduma kwa wateja Bi Adriana Lyamba
amewapongeza wanafunzi hao kwa dhamira yao ya kutaka kujifunza katika ulimwengu
wa technolojia na kuwakaribisha wengine kuhudhuria'
tumefarijika sana kuona wanafunzi toka vyuo vya ndani ya nchi yetu
kama nyie IFM mnafunga safari na kuja kushuhudia hili, hongereni sana
tunawakaribisha wote sio tu wanafunzi bali kila mpenda maendeleo ya technolojia
kutembelea duka hili la kisasa na kujionea au kushauriana na Airtel kufanya
mambo mengi bora zaidi ya ulimwengu wa mawasiliano" alisema Bi
Lyamba.
No comments:
Post a Comment