Tangazo

April 13, 2016

UKATILI WA KIJINSIA SOKO LA TEMEKE STEREO JIJINI DAR BADO CHANGAMOTO NI KUBWA

 Katibu wa Soko la Temeke AStereo, Omary Seif Mangilile akizungumza katika kapmpeni ya kuongeza uelewa dhidi ya ukatili wa kijinsia masokoni iliyofanyika katika soko la Temeke Stereo Dar es Salaam leo asubuhi. Kulia ni Meneja wa Mradi huo wa kupinga ukatili huo, Grace Mateh  kutoka Shirika la Equality for Growth (EfG). 

Hata hivyo katika soko hilo bado kunachangamoto kubwa ya vitendo hivyo vya ukatili wa kijinsia hasa kwenye eneo la wauza mihogo kama ilivyoelezwa na baadhi ya wafanyabiashara katika soko hilo.
 Ofisa Ufuatiliaji na Tathimini wa EfG, Julius Samora akifafanua mambo kadhaa yanayohusu ukatili wa kijinsia katika kampeni hiyo.
Mwezeshaji katika kampeni hiyo Maulid Sufian akiongoza kupokea maswali na kujibu.
Wasanii wa kundi la Machozi la Temeke wakitoa burudani kwenye kampeni hiyo.
Wananchi, wafanyabiasha na wadau wengine wakiwa kwenye kampeni hiyo.
Wananchi, wafanyabiasha na wadau wengine wakiwa 
kwenye kampeni hiyo.
Msanii wa kundi hilo, akionesha umahiri wa kula kwa kutumia mguu wake.
Wasanii wa kundi hilo wakionesha igizo la ukatili wa kijinsia masokoni.
Mfanyabiashara wa soko hilo Mariam Mkula akizungumzia ukatili wa kijinsia unavyofanyika katika soko hilo.
Mfanyabiashara katika soko hilo, Faudhia Maneno akizungumzia ukati wa kijinsia unavyofanyika katika soko hilo.
Bashir Ismaili akichangia jambo kwenye kampeni hiyo.
Hamisi Mnipa akichangia jambo kuhusu ukatili huo ambapo alidai chanzo cha ukatili huo ni wanawake wenyewe kwa kuvaa mavazi yanayoonesha sehemu kubwa ya maungo yao.
Mfanyabiashara katika soko hilo akizungumzia vitendo vya ukatili wa kijinsia katika soko hilo hasa kwa upande wa mama lishe.
Taswira ya jukwaa kubwa.
Muuza chakula katika soko hilo, Neema Saidi akizungumzia changamoto  wanazokumbana nazo za ukatili wa kijinsia hasa pale wanapokwenda kudai fedha kwa wateja baada ya kula chakula.
Vijana katika soko hilo wakichangilia mada zilizokuwa zikitolewa katika kampeni hiyo.

No comments: