Tangazo

April 19, 2016

VICHAKA HATARISHI KATIKA KITUO CHA AFYA BUZURUGA JIJINI MWANZA VYAFYEKWA

Hali ya Usalama katika Kituo cha Afya cha Kata ya Buzuruga kilichopo Manispaa ya Ilemela Mkoani Mwanza imeimarika, baada ya Wakazi wa Kata hiyo wanaounda Kikundi cha Kijamii cha “Ulipo Tupo” kufyeka vichaka vilivyokuwa katika kituo hicho ambavyo vilikuwa vikitumiwa na wahalifu kama maficho yao.

Baada ya kufyeka vichaka hivyo jumamosi iliyopita, Mwenyekiti wa Kikundi hicho, Ndaisaba Aron alisema kuwa vichaka hivyo vilikuwa hatarishi kwa wananchi, wagonjwa pamoja na wahudumu wa Afya katika Kituo hicho, kutokana na kupata malalamiko kwamba vibaka walikuwa wakikimbilia katika vichaka hivyo baada ya kufanya uhalifu.

Hidaya Bashiru ambae ni mwanachama wa kikundi hicho pamoja na Sixtus Ijugo ambae ni Katibu, waliwasihi wananchi wengine kuwa na desturi ya kushiriki katika shughuli za kijamii ikiwemo katika maeneo mbalimbali kama hospitali, shule na kwingineko kwa ajili ya maendeleo yao wenyewe.

Diwani wa Kata ya Buzuruga, Richard Machemba, alijumuika na Kikundi hicho kwa ajili ya kufanya usafi katika Kituo hicho ambapo alipongeza juhudi mbalimbali zinazofanywa na wakazi pamoja na vikundi mbalimbali vya maendeleo katika Kata yake ambapo amewasihi wananchi kuendelea kujitoa kwa ajili ya kushiriki shughuli za maendeleo.
Sikiliza Sauti HAPA Au Bonyeza Play
Tazama Picha HAPA

No comments: