Tangazo

October 11, 2016

DC WA ILALA JIJINI DAR ATOA SOMO KWA WAJUMBE WA BARAZA LA ARDHI

 Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema (kulia), akizungumza na wajumbe wa baraza  la ardhi wa wilaya hiyo Dar es Salaam juzi, wakati wakipeana mikakati ya kazi kwa ajili ya kukabiliana na changamoto ya migogoro ya ardhi.
 Mkutano ukiendelea.
 DC Sophia Mjema (katikati), akiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Mkoa mstaafu wa Dar es Salaam, mama Mary Chipungahelo (kulia) na Katibu Tawala wa wilaya hiyo, Edward Mpogolo.
DC Mjema akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa baraza hilo.

Dotto Mwaibale

WAJUMBE wa Baraza la Ardhi wa Wilaya ya Kinondoni wametakiwa kutobweteka badala yake waende kwa wananchi ili kujua changamoto za ardhi katika wilaya hiyo.

Mwito huo umetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Sophia Mjema Dar es Salaam juzi alipokuwa akizungumza na wajumbe hao ofisini kwake.

"Ninyi ni watu muhimu sana katika kuibua changamoto za ardhi katika kata zetu zote za  wilaya ya Kinondoni nawaomba msiwe watu wa kukaa nendeni kwa wananchi huko kuna changamoto nyingi za ardhi" alisema Mjema.

Mjema aliwataka wajumbe hao kwenda kutoa elimu kwa wananchi ili wajue haki zao kuhusu masuala ya ardhi jambo litakalosaidia kupunguza migogoro ya ardhi.

Aliongeza kuwa migogoro mingi ya ardhi iliyopo katika wilaya hiyo mingi inasabaishwa na wananchi kutojua masuala ya ardhi na elimu.


No comments: