Tangazo

October 9, 2017

MTANDAO WA KIJANI KIBICHI TANZANIA KUUTANGAZA UTALII WA TANZANIA NCHINI THAILAND

 Mtaribu wa ziara hiyo, Mkurugenzi Mwendeshaji wa Kampuni ya Resorce Afrika Limited, Idrissa Songoro akizungumza kuhusu maandalizi ya ziara ya mafunzo ya Wanachama wa Mtandao wa Kijani Kibichi Tanzania (MKIKITA),nchi Thailand inayotarajia kuanza katilati ya mwezi ujao Novemba mwaka huu. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao huo, Adam Ngamange na Mwenyeikiti wa Bodi ya Mkikita, Dk. Kisui . Kisui.UJUMBE wa Wanachama wa Mtandao wa Kijani Kibichi Tanzania (MKIKITA) unaokwenda ziara ya mafunzo nchini Thailand, umejiandaa pia  kwenda kuutangaza utalii wa Tanzania.PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA-KAMANDA WA MATUKIO BLOG


Na Richard Mwaikenda



Akizungumza mjini Dar es Salaam wakati wa kikao cha maandalizi na baadhi ya Wana Mkikita watakaokwenda Thailand, Mtaribu wa ziara hiyo, Mkurugenzi Mwendeshaji wa Kampuni ya Resorce Afrika Limited, Idrissa Songoro amesema kuwa maandalizi ya ziara hiyo kwa upande wa Thailand kwa asilimia kubwa yako tayari.



Amesema kuwa ziara hiyo ya wiki moja Wanamkikita watanufaika kwa mambo mengi, ambapo licha ya kutangaza vivutia mbalimbali vya utalii pia wataonesha utamaduni wa mapishi ya kila aina ya vyakula vya asili vya kitanzania.



Amesema Wanamkikita ambao miongoni mwao ni Wakulima, Wafanyabiashara na Wajasiriamali watapata wasaa wa kubadilishana mawazo na wenzao wa Thailand kwa lengo la kukuza ushirikiano katika masuala ya kibiashara,kilimo cha kisasa na ufugaji wa kisasa.



Songoro amewaasa Wanamkikita kufanya maandalizi  ya uhakika ili wakienda Thailand wanufaike na ziara hiyo na kuwa na mrejesho mzuri watakaporejea nyumbani.



"Kitabia Wathailand wanafanana na Watanzania, kwani ni wakalimu, wapole, waungwana lakini pia ni wachapakazi na wako makini sana katika kila jambo wanalolifanya,"amesema Songoro.



Amesema kuwa Ujumbe huo utapata pia fursa ya kutembelea eneo la viwanda, mashamba ya wakulima pamoja na eneo la utafiti wa kilimo la Chiang Mai na Mji Mkuu wa Bangkok.



"Wathailand wana elimu mkubwa katika nyanja ya uhifadhi wa vyakula na kuviongezea thamani pamoja na kutangaza logo za kibiashara,. Pia wana mbegu za mazao mbalimbali zinazotoa mazao mengi kwa hekali, kwa mfano unaweza kuzalisha kabeji tani 25 kwa heka moja,"amesema Songoro.



Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Mkikita, Dk. Kisui S. Kisui  aliwaasa Wanamkikita kuichangamkia ziara hiyo kwani watakaokwenda watanufaika kwa kupata fursa mbalimbali za maendeleo ikiwemo masuala ya kilimo cha kisasa na biashara.



Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao huo, Adam Ngamange alielezea jinsi Mkikita ilivyopanga kuwaandaa wanajachama watakao kwenda huko kwa kuwapiga msasa kwa kutumia vikao na semina mbalimbali ili wawe na uelewa kwa kujua mambo mbalimbali watakayokwenda kufanya katika ziara hiyo muhimu.



Aliimpongeza Songoro kwa jitihada zake kwa kujitolea kwa moyo mkunjufu kuratibu ziara hiyo itakayokuwa na makubwa kwa Mkikita, Wanachama na Tanzania kwa ujumla.






 Songoro na viongozi wa Mkikita wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Wanamkikita wanaotarajia kwenda Thailand kwa ziara ya wiki moja.
 Dk. Kisui akielezea jinsi Mkikita ulivyojipanga kwa ziara hiyo, itakayowanufaisha wanachama kwa kukutana ana kwa anakwa mazungmzo  na wafanyabiashara na wakulima wa Thailand pamoja na kuingia nao mikataba mbalimbali. 
 Mkurugenzi Mtendaji wa Mkikita, Ngamange akifafanua jambo kwa wajumbe
 Ngamange akiwa na baadhi ya Wajumbe wa Bodi ya Mkikita wakati wa kikao hicho 
 Baadhi ya wajumbe wakiwa katika kikao wakimsikiliza Songoro


 Songoro akifafanua jambo katika kikao hicho
 Ngamange akitoa shukrani kwa Songoro kwa uratibu wa ziara hiyo pamoja na kukubali kushiriki kwenye kikao hicho

 Elizabeth Ndangoba Mkurugenzi wa Fedha na Utawalawa Mkikita
 Catherine Edward Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Mkikita
 Adam Ngamange
 Dk. Kisui akisisitiza jambo alipokuwa akifunga kikao hicho
 Songoro akijadiliana mambo na wajumbe wa Mkikita
 Mjasiriamali Mwambapa akiwa na Ngamange
 Songoro akihojiwa na African Swahili Televisheni
 Ngamange, Rose na Dk Kisui
Songoro akiwa na Mwambapa pamoja na Ngamange

No comments: