Tangazo

February 10, 2012

Hali ya Katibu Mkuu wa TFF Angetile Osiah yazidi kuimarika

 Mhariri Mtendaji wa kampuni ya Free Media Absalom Kibanda akibadilishana mawazo na Katibu Mkuu wa TFF Angetile Osiah ambaye amelazwa Wodi ya Taasisi ya Mifupa (MOI) kwenye hospitali ya Taifa Muhimbili akisumbuliwa na uvimbe sehemu ya kichwa, hali ya Osiah inaendelea vizuri.
HALI ya Katibu mkuu wa Shirikisho la soka Tanzania (TFF) Angetile Osiah imezidi kuimarika na huenda akaruhusiwa wakati wowote kuanzia sasa, imefahamika.

Osiah ambaye amelazwa katika wodi ya Taasisi ya Mifupa (MOI) katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili tangu mwishoni mwa wiki iliyopita akisubuliwa na uvimbe kichwani alisema kwa sasa hali yake inaridhisha.
 
Alisema kutokana na kuimarika kwa afya yake pindi atakapomaliza kutumia dozi maalum kwa ajili ya kusaidia kukausha maji kwenye uvimbe huo.
Kwa hisani ya mamapipiro blog.

No comments: