Tangazo

April 19, 2012

Uharibifu Mkubwa wa Tabaka la Ozone husababisha ongezeko kubwa la Magonjwa mbali mbali

Bi Edith Simtengu Mkurugenzi Msaidisi Rasilimali watu katika Ofisi ya Makamu wa Rais akisoma hotuba ya ufunguzi katika warsha  ya mafunzo kuhusu teknolojia mbadala ya majokofu na viyoyozi na umuhimu wa sekta ya majokofu na viyoyozi katika kulinda tabaka la ozoni iliyofanyika mjini Arusha leo. (picha na Evelyn Mkokoi wa Ofisi ya makamu wa Rais)

Washiriki wa warsha ya mafunzo kuhusu teknolojia mbadala ya majokofu na viyoyozi na umuhimu wa sekta ya majokovu na viyoyozi katika kulinda tabaka la ozoni, wakimsiliza mgeni rasmi hayupo pichani, warsha hiyo imefanyika mjini Arusha leo. (Picha na Evelyn Mkokoi wa Ofisi ya makamu wa Rais)

Akisoma Hotuba kwa niaba ya mgeni rasmi Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha, Bw Julius Achilia ambae ni Afisa mazingira wa Mkoa katika warsha ya mafunzo kuhusu teknolojia mbadala ya majokofu na umuhimu wa sekta ya majokofu na viyoyozi katika kulinda tabaka la ozini. (picha na Evelyn Mkokoi wa Ofisi ya Mkamu wa Rais)

Picha ya pamoja ya washiriki wa warsha ya mafunzo kwa mafundi mchundo wa majokofu na viyoyozi kuhusu teknolojia mbadala ya majokofu na viyoyozi, inayofanyika mjini arusha, (Picha na Evelyn Mkokoi wa Ofisi ya Makamu wa Rais)


Bi Zainab Kuhanwa Afisa Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais akitoa mada kuhusu sensi ya tabaka la ozoni na umuhimu wake kwa washiriki hawapo pichani, katika warsha ya mafunzo kwa mafundi mchundo wa majokofu na viyoyozi kuhusu teknolojia mbadala ya majokofu na viyoyovi, inayofanyika mjini Arusha. (Picha na Evelyn mkokoi wa Ofisi ya Makamu wa Rais)

Afisa Sheria kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais Bw. Isakwisa Lameck, akitoa mada inayohusu Sheria ya Usimamizi wa Mazingira kwa washiriki wa warsha ya mafunzo kwa mafundi mchundo na viyoyozi hawapo pichani mjini Arusha.(Picha na Evelyn Mkokoi wa ofisi ya Makamu wa Rais).
XXXXXXXXXXXXXX
Arusha
Kuongezeka kwa magonjwa ya saratani ya ngozi,uharibifu wa macho maarufu kwa jina la mtoto wa jicho, na upungufu wa uwezo wa mwili kujikinga na maradhi, kumeelezwa kuwa husababishwa kwa kiasi kikubwa na uharibifu wa tabaka la ozone ambapo kunatokana na shughuli za kibinadamu kama vile matumizi ya kemikali haribifu na zisizo rafiki kwa mazingira.

Hayo yameelezwa leo Mjini Arusha katika hotuba ya ufunguzi wa warsha ya mafunzo ya mafundi mchundo wa majokofu na viyoyozi kuhusu teknolojia mbadala ya majokofu na viyoyozi, iliyosomwa na Afisa Mazingira wa Mkoa bw.Julius Achiula kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa.

Akisoma hotuba hiyo,Bw. Achiula ameainisha baadhi ya chemikali hizo kuwa ni methyl bromide, halons na chloroflorocarborns ambazo hutumika kama vipozi katika mafriji, viyoyozi, vifaa vya  kuzima moto, usafishaaji chuma, ufikizaji wa mazao katika maghala na utengenezaji wa magodoro ambazo huleta madhara kwa tabaka la ozone na adhari zake hotokea kwa binadamu, mimea na viumbe hai.

Uhifadhi wa tabaka la ozone umetokana na utekelezaji wa Mkataba wa Montreal na Vienna ambayo Tanzania ni mwanachama.
 
Warsha hiyo inayoratibiwa na Ofisi ya makamu wa rais imehusisha washiriki kutoka, baraza la taifa la Hifadhi na usimamizi wa mazingira NEMC, chuo cha ufundi VETA Moshi, wanahabari,  maafisa mazingira wa mkoa wa arusha na mafundi mchundo.
 
Imetolewa na: Evelyn Mkokoi
Afisa Habari Ofisi ya Makamu wa Rais

No comments: