Tangazo

January 21, 2013

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA, GREGORY TEU AFANYA ZIARA KONYAGI NA TBL


Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Gregory Teu (kulia) akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Kiwanda cha Konyagi cha Tanzania Distilleries Limited (TDL), David Mgwassa kuhusu picha ya watoto wa wakulima wa zao la zabibu wanaosomeshwa na kiwanda hicho, alipotembelea kuona utendaji wa kiwanda hicho, Dar es Salaam juzi.
 Ofisa Biashara wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Athuman Mkungu akiangalia bidhaa mbalimbali zinazozalishwa na kiwanda cha Konyagi.
Naibu Waziri, Teu  (katikati) akitembelea kiwanda cha Konyagi.
 Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Gregory Teu (katikati) akipata maelezo kuhusu uzalishaji wa bidhaa.
 Wafanyakazi wa kiwanda cha Konyagi wakifungasha viroba vya konyagi kiwandani hapo.
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Gregory Teu (kulia) akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Kiwanda cha Konyagi cha Tanzania Distilleries Limited (TDL), David Mgwassa alipotembelea kuona utenddaji wa kiwanda hicho, Dar es Salaam juzi.
 Mtaalamu wa Upishi wa Bia, Kelvin Nkya akimuonesha kompyuta inatumiwa kupikia bia katika kiwanda cha TBL Dar es Salaam.
 Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Gregory Teu (kulia) akipata maelezo kutoka kwa Meneja kiwanda cha Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Martine Calvin (katikati) jinsi bia inavyopikwa kitaalamu alipotembelea kiwanda hicho, Dar es Salaam juzi.
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Gregory Teu (kushoto) akipata maelezo kutoka kwa Meneja kiwanda cha Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Martine Calvin (katikati) kuhusu uzalishaji wa bia unavyofannyika, alipotembelea kiwanda hicho, Dar es Salaam juzi. Kulia ni Mkurugenzi wa Maendeleo ya Viwanda wa wizara hiyo, Genoveva Kilabuko.
 Meneja Uhusiano Mambo ya Nje wa TBL, Emma Oriyo akizungumza wakati wa kumkaribisha Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Gregory Teu.
 Mena wa Kiwanda cha Bia cha TBL, Dar es Salaam, Martine Calvin (kulia) akimpatia zawadi Naibu Waziri.
 Calvin akimpatia zawadi msaidizi wa waziri, Gregory Teu.
 Naibu Waziri Gregory Teu (wa tano kulia) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa TBL
 Mkurugenzi wa Mauzo wa Kiwanda cha Konyagi cha TDL, Joseph Chibehe (kulia) akitoa maelezo kwa Naibu Waziri, Teu.
Mkurugenzi wa Miradi Maalumu wa TBL, Phocus Lasway akielezea mafanikio na changamoto zinazoikabili kampuni hiyo.
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Viwanda wa  Wizara ya Viwanda na Biashara, Kilabuko akizungumza na wafanyakazi wa TBL walipomaliza ziara.. PICHA ZOTE NA KAMANDA WA MATUKIO BLOG

No comments: