Tangazo

September 4, 2013

MTEMVU AKABIDHI TIKETI KWA WATANZANIA ALIOWATAFUTIA KAZI DUBAI

 Mbunge wa Jimbo la Temeke, Abbas Mtemvu (kushoto), akimpatia tiketi ya ndege na nyaraka zinginezo, Nuru Sinna ambaye ametimiza vigezo kwenda kufanya kazi Dubai, Falme za Kiarabu katika hafla iliyofanyika Dar es Salaam hivi karibuni. Wanaoshuhudia  ni  Jaffari Kingwande  (wa pili kulia) ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Bravo Job Centre iliyofanikisha kupata kazi hiyo pamoja wengine wengi watakaokwenda siku za usoni.Wa pili kushoto ni Mohamed Omari Meneja Uhusiano wa kampuni hiyo.
 Mtemvu akionesha nyaraka ikiwemo viza, vibali vya kazi pamoja na tiketi ya Nuru Sunna kwenda Dubai. Jaffari Kingwande  (wa pili kulia) ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Bravo Job Centre iliyofanikisha kupata kazi hiyokufanyakazi.
 Mtemvu akizungumza katika mkuta na waandishi wa habari, Dar es Salaam, kuhusu changamoto mbalimbali ambazo anazipata katika jitihada zake za kuwatafutia kazi watanzania Falme za Kiarabu. Alisema kuwa baadhi ya maofisa wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akiwemo Waziri Belnald Membe wanashiriki kukwamisha jitihada hizo.
 Mtemvu  (mbele katikati) akiwa katika hafla hiyo.
Nuru Sunna (kushoto) akiwa na mdogo wake katika hafla hiyo.

No comments: