Serikali
ya Tanzania imepokea shilingi bilioni 24.1 kutoka Serikali ya Japani kwa ajili
ya shughuli za maendeleo hapa nchini.
Akizungumza
katika hafla hiyo ya kutiliana saini , Waziri wa Fedha Sada Salum Mkuya aliishukuru Serikali
ya Japani kwa kuwa na ushirikiano mzuri
na Tanzania.
“Mkopo
huu utachangia bajeti ya serikali ya mwaka wa fedha wa 2014/2015, na fedha hizo
zitaelekezwa katika sekta ya Maji, Elimu na Afya” alisema Waziri Mkuya.
Mkuya
aliishukuru Serikali ya Japani kwa misaada mbalimbali ambayo imekuwa ikiitoa ambayo
imeleta mafanikio makubwa Tanzania.
Alisema
kuwa kwa mujibu wa taarifa ya Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 ,misaada
hiyo imesaidia kupunguza umaskini na kuongeza kipato kwa wananchi.
Akijibu
swali kuhusu fedha hizo za mikopo kuchelewa kufika, Waziri Mkuya alisema kuwa changamoto
kubwa ambayo Serikali imekuwa ikiipata ni kutokana na taratibu za sera za nchi husika ambapo kila nchi wana
sera zao.
Kwa
upande wake Balozi wa Japan Nchini Tanzania Masaki Okada alisema kuwa msaada
huo unahusiana na ushirikiano wa pamoja na Benki ya Dunia katika mkopo wa kumi
na moja wa kusaidia kupunguza umaskini ambao umekuwa ukitolewa tangu mwaka
2001.
Mikopo
hiyo imekuwa ikitolewa kwa masharti ya mkataba wa mkopo nafuu wa riba ya
asilimia 0.01 kwa Serikali hapa nchini.
Balozi
Okada alisema kuwa nchi yake imekuwa ikitoa mikopo mabalimbali ili kusaidia Serikali
ya Tanzania katika kupunguza umaskini ambapo misaada hiyo imekuwa ikitumika
kufuatana na GBS hapa Tanzanaia kwa kutoa fedha moja kwa moja ambazo zinalenga kuharakisha
juhudi za kupunguza umasikini hususani MKUKUTA.
Naye
Mwakilishi wa Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Japani (JICA) nchini
Yasunori Onioshi alisema kuwa shirika lake litaendelea kushirikiana na
Serilkali ya Tanzania katika kusaidia bajeti yake kwani Tanzania inakua kwa
haraka na mahitaji yake yanaendelea kuongezeka kila mara.
Makampuni
ya Kijapani yanayofanya kazi na Serikali ya Tanzania ni pamoja na Kampuni ya
Sigara (TCC) inayomilikiwa na Kampuni ya Kimataifa ya Tumbaku ya Kijapani,
Panasonic Energy Tanzania na JICA.
Hali
ya hewa ya Dodoma ni baridi na majadiliano kuhusu Bajeti ya Serikali yameanza
na yanaendelea.
Imetolewa na:
Msemaji Mkuu
Wizara ya Fedha
16/06/2014
No comments:
Post a Comment