Tangazo

June 24, 2014

UZINDUZI WA FILAMU YA ‘I LOVE MWANZA’ UWANJA WA CCM KIRUMBA MWANZA

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe (wa pili kushoto), akizindua filamu mpya iitwayo ‘I Love Mwanza’ iliyoandaliwa na Lake Zone Youth Empowerment Foundation kwa kushirikiana na Tropical Media Tanzania Ltd, katika hafla iliyofanyika kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza Jumapili Juni 22.2014. Wanaoshuhudia ni Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF), Simon Mwakifwamba (kulia), Rais wa Bongo Movie, Steven Mengele ‘Steve Nyerere (kushoto) na Mwenyekiti wa Chama cha Sanaa za Maonyesho na Waigizaji Tanzania (TDFAA), Mkoani Mwanza, Anitha Kagemulo (wa pili kushoto). PICHA NA JOHN BADI wa Daily Mitikasi Blog
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe akiuhutubia umati wa wananchi waliofurika katika Uwanja wa CCM Kirumba, baada ya kuzindua filamu mpya iitwayo ‘I Love Mwanza’, iliyoandaliwa na Lake Zone Youth Empowerment Foundation kwa kushirikiana na Tropical Media Tanzania Ltd, jijini Mwanza Jumapili Juni 22.2014.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe na Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF), Simon Mwakifwamba (kulia), wakilisakata rhumba lililokuwa likiporomoshwa na Bendi ya The African Stars ‘Twanga Pepeta’, katika hafla ya uzinduzi wa filamu mpya ya ‘I love Mwanza’, uliofanyika kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza Jumapili Juni 22.2014.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe akilakiwa na umati wa wananchi kabla ya kuzindua filamu mpya ya ‘I love Mwanza’, uliofanyika kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza Jumapili Juni 22.2014.

No comments: