Tangazo

March 28, 2012

RAIS KIKWETE AFUNGUA WARSHA YA MIKAKATI YA KUONDOA UMASKINI JIJINI DAR LEO

Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa REPOA Profesa Esther Mwaikambo, Mkurugenzi Mtendaji wa REPOA Profesa Samuel Wangwe, Balozi wa Uholanzi nchini Dkt Ad Koekkoek, Katibu Mtendaji a Tume ya Mipango Dkt Phillip Mpango na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mh Saidi Meck Sadick muda mfupi kabla ya kuondoka hoteli ya White Sands Hotel alikofungua warsha ya siku mbili ya Utafiti.

Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Profesa Ibrahim Lipumba baada ya picha ya pamoja na washiriki wa warsha ya siku mbili ya utafiti juu ya mageuzi ya kuondoa umaskini.

Profesa Do Duc Dinh toka Vietnam akitoa mada ya jinsi nchi yake ilivyofanikiwa kuondoa umaskini warsha ya siku mbili ya utafiti juu ya mageuzi ya kuondoa umaskini nchini.

Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akimpongeza Katibu Mtendaji a Tume ya Mipango Dkt Phillip Mpango  kwa mada nzuri. Kati yao ni  Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa REPOA Profesa Esther Mwaikambo na kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa REPOA Profesa Samuel Wangwe na Balozi wa Uholanzi nchini Dkt Ad Koekkoek.

Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akimsikiliza  Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango Dkt Phillip Mpango  akitoa mada ya ufunguzi wa warsha hiyo ya siku mbili ya REPOA. Wengine toka shoto  Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa REPOA Profesa Esther Mwaikambo na kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa REPOA Profesa Samuel Wangwe na Balozi wa Uholanzi nchini Dkt. Ad Koekkoek.

Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akipongezwa kwa hotuba nzuri ya ufunguzi na  Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa REPOA Profesa Esther Mwaikambo na kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa REPOA Profesa Samuel Wangwe. PICHA/IKULU

No comments: