Tangazo

May 19, 2012

Tanzania yawasilisha Maoni kuhusu Masuala ya Kilimo na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Bi Emelda Taikwa Adam, Afisa Mazingira Mwandamizi kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais Akiwasilisha maoni ya Tanzania katika masuala ya Kilimo na mabadiliko ya Tabia nchi, katika mkutano wa sayansi ya Taaluma ya mabadiliko ya tabia nchi unaendelea mjini Bonn Ujerumani (Picha na Evelyn Mkokoi)

Washiriki Kutoka Tanzania Bi Fauzia Haji (kulia), kutoka Idara ya Mazingira Zanzibar, Bi Imelda Adam (Katikati)  Afisa Mazingira mwandamizi Ofisi ya Makamu wa Rais, na Bw. Ladslaus Kyaruzi Afisa Mazingira Mwandamizi kutoka Ofisi ya Makamo wa Rais wakijiandaa kuwasilisha mada kwa niaba ya nchi za Afrika katika mkutano wa Sayansi na Taaluma ya Mabadiliko ya Tabia Nchi unaendelea Mjini Bonn Ujerumani kuhusu Madhara yatokanayo na mabadiliko ya tabia nchi.
************************
EVELYN MKOKOI
AFISA HABARI OMR
BONN UJERUMANI

Tanzania kama nchi nyingine zinazoendelea imepata fursa ya kuwasilisha maoni yake  kuhusu kilimo katika kuhimli  mabadiliko ya Tabia nchi katika mkutano kimataifa wa 36 wa sayansi na taaluma ya mabadiliko ya tabia nchi, unaendelea mjini Bonn Ujeremani.

Akiwasilisha maoni hayo, katika Mkutano huo Afisa Mazingira Mwandamizi kutoka Ofisi ya makamu wa Rais Bi Emelda Taikwa Adam ameeleza kuwa, nchi zinazoendelea ikiwemo Tanzania zinatakiwa kuangalia zaidi katika kuhimili mabadiliko ya tabia nchi ili kuweza kuongeza uzalishaji na kuhakikisha usalama wa chakula kupitia sekta ya kilimo kwani ndo uti wa mgongo wa Taifa.

Bi Emelda aliongeza kuwa, katika kuhimili mabadiliko ya Tabia nchi Tanzania kupitia sekta ya kilimo na tafiti zilizokwisha fanyika kuonyesha kuwa kuna matumizi salama ya mbegu zinazohimili ukame, pamoja na matumizi sahihi ya kilimo cha umwagiliaji, na kuna kila sababu ya matumizi ya teknolojia zaidi ya kisasa na kujenga uwezo kwa wakulima wa kawaida ili kuweza kuhakikisha usalama wa chakula.

“Tafiti zinaonyesha kuwa kilimo huchangia 13% katika kuzalisha gesi joto hivyo basi kuna umuhimu mkubwa wa kuingiza masuala ya kilimo katika kuhimili mabadiliko ya tabia nchi, kwa sababu nchi zinazoendelea ikiwemo Tanzania hutegemea kilimo alisisitiza.”

Akizungumzia athari za mabadiliko ya Tabia nchi katika sekta ya kilimo bi Emelda amesema kuwa, kupungua kwa mvua kunakopelekea ukame nchini na kuongezeka kwa gesi joto kumeathiri kwa kiasi kikubwa sana sekta ya kilimo, na katika kupunguza gas joto katika kilimo kunahatarisha usalama wa chakula na kupoteza ardhi kwa wenyeji.

Aliongeza kuwa pamoja na kwamba sekta ya kilimo imekuwa na mikakati mbalimbali inayotekelezeka katika kuhimili mabadiliko ya tabia nchi, Tanzani inatakiwa kuwa na mfumo ambao utahakikisha kuwa upunguzaji wa gesi joto katika kilimo unatokana na jitihada za kuhimili mbadiliko ya tabia nchi.

No comments: