Tangazo

May 19, 2012

VIJANA 'WAJIFUA' TAYARI KWA MPAMBANO WA MASUMBWI KINONDONI




Katika picha ni baadhia ya mabondia chipukizi wa bigright boxing na mwalimu wao IBRAHIM KAMWE wakimalizia mazoezi yao ya mwishomwisho kwa ajili ya mpambano wa ngumi unaotegemewa kufanyika Jumapili 20/05/2012 katika ukumbi wa Vijana Hall kinondoni wakisindikiza pambano la ubingwa wa taifa wa Bantam weight chini ya usimamizi wa TPBO kati ya RAMADHAN KUMBELE na JAMES MOKIWA raundi kumi.

Vijana hao wameahidi kuonesha mchezo mzuri wa ushindi 'kama ilivyo kawaida yetu ushindi kwetu ibada'

Mabondia hao wanaotegemea kupima uzito leo Jumamosi 19 katika ukumbi wa STEREO Club-Kinondoni na Heavy weight Anord'biggie'120kg v/s Karim 'big paquiao' 118kgs raundi sita, feather weight - Doi Miyeyusho v/s Jumanne Mtengela, Light weight Jafar Majia v/s Daudi Muhunzi, Fly weight-Sadat Miyeyusho v/s Swed Hassan, Martin Richard v/s Yohana Thobias na mapambano mengi mengineyo yakiwemo ya watoto na Burudani toka kwa KARAPINA,MAKHIRIKHIRI WA KIBONGO NA TID.

Mapambano haya yote yameratibiwa na Tasenga na BigRight Promotion kwa lengo la mfululizo wa mapambano ya kuinua vipaji vya mabondia wa Tanzaniana kutafuta mabingwa wa taifa kabla ya kimataifa.

No comments: