Tangazo

June 4, 2012

CCM YAITEKA SONGEA

Chama Cha Mapinduzi (CCM) leo kimeiteka Songea baada ya umati wa wananchi wa mji huo kujitokeza katika mkutano wa hadhara wa CCM uliohutubiwa na Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye  kwenye Uwanja wa Majimaji mjini Songea mkoani Ruvuma. Pichani, Nape akiwasalimia wananchi baada ya kuwasili kwenye uwanja huo. Kushoto ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Ruvuma Cornel Msuha. (Picha na  Bashir Nkoromo).

Nape akizindua mradi mabanda 119 ya biashara eneo la Mshengano,Songea. Vibanda hivyo vya CCM vimejengwa na CCM kwa sh. milioni 206.
Nape akifungua Shina la wakereketwa wa CCM, wafanyabiashara kwenye mabanda ya Chama Kata ya Mshengano, Songea.


Nape akishiriki kucheza ngomabaada ya kuwasili Uwanja wa MajiMaji.

Kina mama wakigara gara chini mbele ya Nape (jukwaani) baada ya kuingiwa na hotuba yake.

Nape akipita kwenye kanga zilizotandikwa na kina mama waliovutiwa na hotuba yake.

Mkazi wa Kata ya Tanga, mjini Songea, Kamanda Nico, akimsalimia Nape katika mapokezi hayo.

No comments: