Tangazo

August 29, 2012

NAIBU WAZIRI WA AFYA NA USTAWI WA JAMII, DK. RASHID AKAGUA MAENDELEO WILAYANI RUFIJI

 Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Rufiji, Dk. Seif Rashid  (Kulia)  akisalimiana na akina mama wa Kijiji cha Mtanza baada ya kumalizika kwa mkutano na wananchi wa eneo hilo wakati wa  ziara ya kuwashukuru wananchi kwa kumchagua kuwa mbunge pamoja na kuwaeleza majukumu mengine aliyonayo sasa ya unaibu waziri.

Dk Rashid akihutubia katika mkutano uliofanyika katika Kijiji cha Mtanza jimboni humo juzi. Kulia ni Diwani wa Kata ya Mwaseni, Athuman Mbange (CUF) na kushoto ni Mwenyekiti wa Kijiji cha Mtanza.

Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Rufiji, Dk. Seif Rashid  (wa pili kushoto) akiwa na baadhi ya viongozi wa Kata ya Mwaseni, akikagua maendeleo ya ujenzi wa chumba cha darasa wa ziara ya kuwashukuru wananchi kwa kumchagua kuwa mbunge pamoja na kuwaeleza majukumu mengine aliyonayo sasa ya unaibu waziri.

Bibi Fatuma Mazengo akiangua kilio mbele ya waziri alipokuwa akieleza jinsi mkwe wake na mjuu wake walivyouawa kinyama na Askari wa Wanyapori katika Hifadhi ya Mbuga ya Selou mpakani mwa kiji cha Mloka, Rufiji. Watu hao waliuawa walipokwenda kuvua samaki katika ziwa la Mzizimia kwa ajili ya kitoweo.


Akina mama wa Kijiji cha Mibuyu Saba  wakisikiliza kwa makini hotuba ya Waziri.

Mkazi wa Kijiji cha Mtanza, Yusufu Nyamgumi, akihoji kwenye mkutano kitendo cha Diwani wao, Athuman Mbange (CUF) kutokuwa na tabia ya kuwatembelea kujua matatizo yao. (PICHA ZOTE NA KAMANDA MWAIKENDA)

No comments: