Tangazo

September 16, 2013

Wateja wa Airtel money kunufaika na huduma za kibenki

Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel,  Bi. Beatrice Singano Mallya
• Wateja wanaweza kuamisha pesa kutok kwenye akaunti zao za benki kwenda kwenye akaunti ya Airtel money masaa 24 siku 7 za wiki.


• Ni njia salama, rahisi ya kupata pesa kupitia kutoka Airtel

Airtel Tanzania kupitia huduma yake ya Airtel money imeanzisha ushirikiano na benki mbalimbali nchini na kuwawezesha wateja wake kuhamisha pesa kutoka kwenye benki akaunti zao na kuziweka kwenye akaunti ya Airtel money

Banki ambazo zimeingia katika ushirikiano huo na Airtel ni pamoja na Tanzania Postal Bank, Bank of Africa, Kenya Commercial Bank, Barclays Bank, Akiba Commercial Bank, Exim Bank, Amana Bank, Mkombozi Commercial Bank na Standard Chartered bank.

Akiongea juu ya ushirikiano huo Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel,  Bi. Beatrice Singano Mallya alisema” kuanzishwa kwa mpango huu wa huduma ya Airtel money na za kibenki kutawawezesha wateja Airtel kutoa pesa kwenye akaunti zao za benki na kuziweka kwenye simu zao yani akaunti ya Airtel money kirahisi bila kutembelea ofisi za benki.  

Huduma ya Airtel Money ni suluhisho la huduma za kifedha ikiwa na zaidi ya mawakala 20,000 , kupitia mtandao wetu mpana ulioeneea nchi nzima tunauhakika wa kuwafikia watu  engi zaidi hasa wa maeneo ya vijijini”

Tunaamini ushirikiano na benki zingine kutaendelea kuwaletea wateja wa huduma ya Airtel money ufanisi na urahisi wa upatikanaji wa fedha kutoka kwenye benki zao wakati wote mahali popote nchi nzima.”

Mallya aliendelea kusema Airtel imedhamiria kutoa huduma za kiubunifu kwa watanzania kwani tunatambua tecknologia ya simu inazidi kukua na kuunganisha watu na kubadili maisha ya jamii.  

Huduma ya Airtel money inatoa mwanya kwa makampuni, watoaji huduma za kitechnologia inawezesha huduma za malipo na kukuza huduma za kifedha nchini. Airtel imejipanga kutoa huduma za kifedha na kuiwezesha kuwa ya mafanikio aliongeza Mallya.

Akiongea kuhusu ushirikiano meneja huduma wa Airtel Money Bw , Asupya Nalingingwa Alisema”  unafuraha kuingia kwenye makubaliano haya ya ushirikiano wa kutoa huduma za kifedha na benki hizi tofauti ambapo kwetu ni nafasi nzuri ya kuendelea kuboresha huduma za kifedha nchini na kuwafikia wateja wa benk hizi na wateja wa Airtel wasio na huduma ya benki hizo maeneo ya karibu.

Ili kupata orodha ya huduma za benki husika mteja anatakiwa kupiga namba zifuatazo na kufuata maelezo Tanzania Postal Bank –*150*21#, Bank of Africa –*150*13#, Kenya Commercial Bank –*150*22#, Barclays
Bank –*150*20#, Akiba Commercial Bank –*150*10#, Exim Bank –*150*11#, Amana Bank –*150*12#, Mkombozi Commercial Bank –*150*06# , Standard Chartered Bank – *150*65#

Huduma ya Airtel money inawawezesha wateja kulipia bili zao, kutuma na kupokea pesa na kufanya miamala mbalimbali, huduma hii inapatikana kwa wateja wa malipo ya awali na ya kabla , kujiunga na huduma hii ni bure kwa kupita maduka ya Airtel na mawakala nchi nzima.  Mpaka sasa Airtel Money  inamawakala zaidi ya 20,000 Wanaotoa huduma za kifedha kwa wateja nchini. Airtel inatoa huduma ya Airtel money kwa msharika na watu binafsi kama njia mbadala ya malipo.


Airtel pia kupitia Airtel Money kwa sasa imezindua promosheni mpya ya Hakatwi mtu hapa nayowawezesha wateja wa Airtel kutuma na kutoa pesa bila makato yoyote popote pale nchini.

No comments: