Tangazo

October 8, 2014

TAMASHA KUBWA LA KARIBU MUSIC FESTIVAL KUFANYIKA BAGAMOYO



 Meneja wa tamasha la Karibu Music Festival, Richard Lupia akizungumza katika mkutano na waandishi wa Habari Dar es Salaam hii leo juu ya maandalizi ya tamasha hilo.
 Meneja wa tamasha la Karibu Music Festival, Richard Lupia akizungumza katika mkutano na waandishi wa Habari Dar es Salaam hii leo juu ya maandalizi ya tamasha hilo. Kushoto ni Mratibu wa Tamsha, Issam Ramadhan na Kulia ni Afisa Habari wa Karibu Music Festival, Said Hashim.


Meneja wa tamasha la Karibu Music Festival, Richard Lupia akifafanua jambo katika mkutano na waandishi wa Habari Dar es Salaam hii leo juu ya maandalizi ya tamasha hilo. Kushoto ni Mratibu wa Tamsha, Issam Ramadhan
 ********
Na Father Kidevu Blog
Tamasha kubwa la Karibu International Music Festival, linataraji kufanyika nchini kwa mara ya kwanza katika Pwani ya viwanja vya Taasisi ya Sanaa Bagamoyo (TASUBA).

Waratibu wa Tamasha hilo Karibu Cultural Promotions kupitia kwa Meneja wa Onesho hilo, Richard Lupia, amesema litafanyika kwa siku tatu kuanzia Novemba 7-9 Mwaka huu wa 2014.

Lupia amesema vikundi zaidi ya 30 na wasanii zaidi ya 500 kutoka kila kona ya dunia wanaopiga muziki wa dansi,Reggae, Hip Hop, Taarab, Ngoma za Asili, Bongofleva na Ghani wanataraji kushiriki.

“Lengo kuu la Tamasha, pamoja kukazia katika kurasimisha tasnia ya muziki kuwa na umakini zaidi, lakini kingine ni kukuza uchumi wa eneo husika la Bagamoyo ambalo ni la kihistoria, pamoja na kuhakikisha sanaa ya asili ya mtanzania inapata kuonekana katika jukwaa la kimataifa,”alisema Lupia.

Tofauti na matamasha mengine yaliyowahi kufanyika Tanzania Bara, hili
litakuwa likitumia ala kwa asilimia mia moja, wasanii wote watakaoshiriki,
watalazimika kutumia muziki wa ala kuimba na sio Playback.

Ukiachana na burudani, wasanii pia watapata nafasi ya kujifunza jinsi ya
kuunadi muziki wao duniani kwa njia mbali mbali ambako kutakuwa na warsha kutoka kwa wataalamu mbali mbali toka pembe zote za dunia.

Tamasha litakuwa likiendeshwa mchana na usiku ambapo mchana sanaa za michoro, mavazi na kuchonga zitakuwa zikioneshwa eneo la tamasha huku semina na mijadala ya jinsi ya kuupeleka muziki wa tanzania katika hatua nyingine za kimaendeleo zikiwa zinaendelea.

Mpaka sasa zaidi ya vikundi 100 vimeomba kushiriki tamasha kutoka pembe mbali mbali za dunia, tuko katika kuvichuja na kuangalia ubora wao, na Mungu akipenda, wiki ijayo tutakuja tena kuwaambia majina ya wasanii watakaoshiriki tamasha hili linalotarajiwa kuwa kubwa kuliko yote Afrika ya Mashariki.

Lengo la kuja hapa mbele yenu kwa leo lilikuwa ni kuwajulisha kuhusiana na
hili na kutoa rasmi ombi letu kwenu la kusambaza ujumbe kuhusiana na fursa hii kwa wasanii wetu kujifunza kutoka kwa wenzetu, jinsi wenzetu kutoka nchi zinazoendelea, wanavyofaidika na sanaa yao ili na sisi tuweze kujikomboa.

Tunatanguliza shukrani zetu kwa kuhudhuria kwanza, lakini kingine tunaomba ushirikiano, bado sisi ni wachanga, tujitahidi kuhakikisha kwamba muziki wa Tanzania unafika katika kilele cha mafanikio.

No comments: