Tangazo

November 19, 2014

ZIARA YA KINANA NACHINGWEA

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana (katikati) akiongozana na Mbunge wa Jimbo la Nachingwea na Waziri wa Mambo ya Ndani Ndugu Mathias Chikawe (kulia) pamoja na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Nachingwea Ndugu Albert Mnari kuelekea kwenye shamba la ushirika Mkotokuyana  wilaya ya Lindi Vijijini tayari kwa kushiriki shughuli za kilimo.
 Kikundi cha Wakulima cha Umoja Rika wakiinua majembe juu kama ishara ya kumkaribisha Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana aliyefika kwenye shamba hilo la ushirika la Mkotokuyana wilaya ya Nachingwea.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na wakulima wa kikundi cha Umoja Rika kilichopo Mkotokuyana ,Nachingwea.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwasalimia wakulima wa kikundi cha Umoja Rika kilichopo Mkotokuyana,Nachingwea mkoani Lindi.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiendesha treka kulima shamba la ushirika la Mkotokuyana huku akiwa amempakia Mbunge wa Jimbo la Nachingwea Ngugu Mathias Chikawe.
  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kung'oa visiki katika shamba la Mkotokuyana  wilayani Nachingwea.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wananchi wa kijiji cha Mandai ambao walieleza shida ya maji,zahanati pamoja na ofisi ya Serikali .
  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki ujenzi wa jiko la kisasa la shule ya sekondari ya Nachingwea High School .
  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiangalia majiko ya kisasa ya shule ya sekondari ya Nachingwea.
  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wajumbe wa halmashauri kuu ya wilaya ya Nachingwea.
  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wananchi wa kijiji cha Naipanga ambapo alikagua na kushiriki ujenzi , Katibu mkuu wa CCM aliwaambia wananchi wawe mstari wa mbele katika kuchangia maendeleo yao.
  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki ujenzi wa ofisi ya serikali ya kijiji cha Naipanga Nachingwea.
  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiangalia korosho kwenye ghala ambalo hapo awali ilikuwa kiwanda cha korosho cha Nachingwea .
 Sehemu ya shehena ya Korosho.
 
 Kiwanda cha Mafuta ya Ufuta Ilulu Nachingwea ambacho sasa kinatumika kama ghala ya kuhifadhia vifaa vya umeme.
 Wananchi wa Nachingwea wakishangilia ujio wa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana ambaye yupo kwenye ziara ya kujenga na kukiimarisha chama mkoani Lindi.

 Katibu wa Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa Nachingwea ambapo aliwaambia upinzani umepotea kabisa hivyo wasipoteze muda wao kushabikia
 Wananchi wakifurahia hotuba ya Katibu wa Nec Itikadi na Uenezi Nape Nnauye.
 Mama akichukua matukio kwa simu yake wakati mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Soweto wilaya ya Nachingwea.
 Wananchi wakifuatilia mkutano nje ya senyenge ya uwanja wa mikutano wa Soweto wilayani Nachingwea.
 Mbunge wa Jimbo la Nachingwea na Waziri wa Mambo ya Ndani akielezea utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM 2010  katika jimbo lake kwenye mkutano uliofanyika kwenye viwanja vya Soweto, Nachingwea.
 Bibi Esha Kanduru mwenye umri wa 89 ambaye alishiriki harakati za uhuru na kujiunga na TANU mwaka 1957 akifuatilia kwa makini mkutano wa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kwenye uwanja wa Soweto, Nachingwea.
  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa Nachingwea ambapo aliwaambia kuwa CCM itakuwa wakali pindi serikali inapokosea mambo na kuchelewa kuchukua hatua, kwani maumivu na mateso wanapata wananchi, akizungumzia kusikitishwa kwake kwenye viwanda vya korosho ambavyo vimegeuzwa kuwa maghala na hakuna mtu serikalini amestuka kwa zaidi ya miaka kumi sasa.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akizungumza na Mbunge wa Jimbo la Nachingwea Ndugu Mathias Chikawe wakati wa mkutano wa CCM mjini Nachingwea kwenye viwanja vya Soweto.
  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akionyesha kadi za wanachma kutoka CUF waliojiunga rasmi na CCM wilayani Nachingwea.


No comments: