Mfanyabiashara wa Soko la Jipya la
Kawe, Grace Pascal Kalengela (wa pili kulia), ambaye aliibuka mshindi wa
Droo ya tatu ya promosheni ya Airtel Yatosha Zaidi akiwa mwenye furaha, kabla
ya kukabidhiwa zawadi ya gari jipya aina ya Toyota IST lililosajiliwa kwa namba
T 783 DCZ katika hafla iliyofanyika eneo la Kawe jijini Dar es Salaam jana. Kulia
ni Meneja Biashara wa Airtel Kanda ya Dar es Salaam, Fredrick Mwakitwange.
xxxxxxxxxxxxxxxx
Dar es Salaam, Februari 24, 2015
MWANAMKE mchuuzi wa mboga mboga katika Soko jipya la Kawe jijini Dar es
Salaam, Grace Pascal Kalengera, jana alikuwa miongoni mwa wakazi watatu wa Dar
es Salaam waliokabidhiwa zawadi zao baada ya kushinda promosheni ya Airtel
Yatosha Zaidi.
Ijumaa iliyopita, Grace alipigiwa simu na Balozi wa Airtel Yatosha Zaidi,
mwigizaji maarufu nchini, Lulu, baada ya namba yake kuwa miongoni mwa washindi
kwenye droo iliyochezeshwa makao makuu ya Airtel jijini Dar es Salaam na
kushuhudiwa na mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kuigiza nchini.
Siku nne tu baadaye, leo Jumanne, Meneja Masoko wa Airtel, Frederick Mwakitwange,
alimkabidhi gari lake mama huyo aliyeonekana wazi akiwa na furaha isiyo kifani.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Mwakitwange alisema: “Sisi Airtel, tunafarijika
sana tunapowaona washindi wakimiminika ofisini kwetu kila wiki kujichukulia
zawadi zao. Na kwa ukweli zawadi ya gari si zawadi ndogo kwa wengi miongoni
mwetu.
“Tuliamua kwa makusudi kabisa kutoa magari kama zawadi kwa washindi kwa lengo
la kuonyesha nia yetu ya kuboresha na kuyabadili maisha ya Watanzania.”
Mbali na Grace, washindi wengine waliokabidhiwa magari yao ni pamoja na John
Freddy Kiwale mkazi wa Kinondoni ambaye pia ni wakala wa Airtel Money na
Donald Fred Baruti mfanyabiashara wa Mwembechai.
Meneja Uhusiano wa Airtel, Jackson Mbando, alitoa wito kwa wateja wa kampuni
hiyo kuendelea kutumia huduma za Airtel Yatosha Zaidi waweze kupata nafasi ya
kujishindia magari.
“Kama mnavyoona, hata mawakala wa Airtel Money wanaweza kushinda. Hii ni kwa
sababu tu kwamba nao pia ni wateja wetu. Inafahamika kuwa kuna vigezo na masharti
katika kushiriki na sisi tunazingatia sana hilo,” alisema Mmbando.
Washindi wengine wa wiki iliyopita watakaopewa magari ya oleo ni Simon Grayson
(Yombo, Kisiwani), Bilal Juma Mlendela (Tabata) na Maxbeth Isack Manene
(Tabata Segerea), kisha mkazi na mkulima kutoka Bukoba, Kajala Kokutima Said,
naye atapewa gari wiki hii.
Tayari magari 17 kati ya 60 yamekwishapata wamiliki wake wapya.
|
No comments:
Post a Comment