Tangazo

February 25, 2015

Wateja watatu Dar wakabidhiwa magari na Airtel baada ya kuibuka washindi

Mfanyabiashara  wa Soko la Jipya  la Kawe,  Grace Pascal Kalengela (wa pili kulia), ambaye aliibuka mshindi wa Droo ya tatu ya promosheni ya Airtel Yatosha Zaidi akishangiliwa na wafanyabiashara wenzake sokoni hapo, kabla ya kukabidhiwa zawadi ya gari jipya aina ya Toyota IST lililosajiliwa kwa namba T 783 DCZ katika hafla iliyofanyika eneo la Kawe jijini Dar es Salaam jana.
Meneja Biashara wa Airtel Kanda ya Dar es Salaam, Fredrick Mwakitwange (kushoto), akikabidhi mfano wa ufunguo wa  gari kwa mshindi wa droo ya tatu ya promosheni ya Airtel Yatosha Zaidi, Grace Pascal Kalengela  wakati wa  kumkabidhi  gari jipya aina ya Toyota IST lililosajiliwa kwa namba T 783 DCZ katika hafla iliyofanyika katika eneo la Kawe jijini Dar es Salaam jana. Wa (pili kushoto) ni mume wa mshindi huyo, Daudi Mayunga na (kulia) ni Meneja Uhusiano wa Airtel, Jackson Mmbando.
Mfanyabiashara  wa Soko la Jipya  la Kawe,  Grace Pascal Kalengela (wa pili kulia), ambaye aliibuka mshindi wa Droo ya tatu ya promosheni ya Airtel Yatosha Zaidi akiwa mwenye furaha, kabla ya kukabidhiwa zawadi ya gari jipya aina ya Toyota IST lililosajiliwa kwa namba T 783 DCZ katika hafla iliyofanyika eneo la Kawe jijini Dar es Salaam jana. Kulia ni Meneja Biashara wa Airtel Kanda ya Dar es Salaam, Fredrick Mwakitwange.
xxxxxxxxxxxxxxxx
 
 Dar es Salaam, Februari 24, 2015

MWANAMKE mchuuzi wa mboga mboga katika Soko jipya  la Kawe jijini Dar es Salaam, Grace Pascal Kalengera, jana alikuwa miongoni mwa wakazi watatu wa Dar es Salaam waliokabidhiwa zawadi zao baada ya kushinda promosheni ya Airtel Yatosha Zaidi.

Ijumaa iliyopita, Grace alipigiwa simu na Balozi wa Airtel Yatosha Zaidi, mwigizaji maarufu nchini, Lulu, baada ya namba yake kuwa miongoni mwa washindi kwenye droo iliyochezeshwa makao makuu ya Airtel jijini Dar es Salaam na kushuhudiwa na mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kuigiza nchini.

Siku nne tu baadaye, leo Jumanne, Meneja Masoko wa Airtel, Frederick Mwakitwange, alimkabidhi gari lake mama huyo aliyeonekana wazi akiwa na furaha isiyo kifani.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Mwakitwange alisema: “Sisi Airtel, tunafarijika sana tunapowaona washindi wakimiminika ofisini kwetu kila wiki kujichukulia zawadi zao. Na kwa ukweli zawadi ya gari si zawadi ndogo kwa wengi miongoni mwetu.

“Tuliamua kwa makusudi kabisa kutoa magari kama zawadi kwa washindi kwa lengo la kuonyesha nia yetu ya kuboresha na kuyabadili maisha ya Watanzania.”

Mbali na Grace, washindi wengine waliokabidhiwa magari yao ni pamoja na John Freddy Kiwale  mkazi wa Kinondoni ambaye pia ni wakala wa Airtel Money na Donald Fred Baruti mfanyabiashara wa Mwembechai.

Meneja Uhusiano wa Airtel, Jackson Mbando, alitoa wito kwa wateja wa kampuni hiyo kuendelea kutumia huduma za Airtel Yatosha Zaidi waweze kupata nafasi ya kujishindia magari.

“Kama mnavyoona, hata mawakala wa Airtel Money wanaweza kushinda. Hii ni kwa sababu tu kwamba nao pia ni wateja wetu. Inafahamika kuwa kuna vigezo na masharti katika kushiriki na sisi tunazingatia sana hilo,” alisema Mmbando.

Washindi wengine wa wiki iliyopita watakaopewa magari ya oleo ni Simon Grayson (Yombo, Kisiwani), Bilal Juma Mlendela (Tabata) na  Maxbeth Isack Manene (Tabata Segerea), kisha mkazi na mkulima kutoka Bukoba, Kajala Kokutima Said, naye atapewa gari wiki hii.

Tayari magari 17 kati ya 60 yamekwishapata wamiliki wake wapya.

No comments: