Tangazo

March 19, 2015

MADIWANI WA MANISPAA YA LINDI WATEMBELEA MRADI MAPINGA SATELLITE WA UTT-PID ULIOPO BAGAMOYO

Diwani wa Kata ya Nachingwe, Lindi Mjini, Omary Chitanda (katikati) akiuliza swali kwa mtaalamu wa mradi huo
Diwani wa Kata ya Nachingwe, Lindi Mjini, Omary Chitanda (katikati) akiuliza swali kwa mtaalamu wa mradi huo.

*Taasisi ya Miradi na Maendeleo ya Miundombinu (UTT-PID) ilianza kazi zake Julai 1, 2013. Taasisi hii ilirithi kazi za miradi zilizokuwa zinafanywa na Taasisi mama yaani UTT.

Andrew Chale wa Mo dewji blog aliyekuwa Bagamoyo

Baadhi ya Madiwani wa Manispaa ya Lindi Machi 17, wametembelea miradi mbali mbali ya UTT-PID iliyopo Dar es Salaam ikiwemo ule wa Bagamoyo wa New Mapinga Satellite.
Madiwani hao waliweza kujifunza mambo mbalimbali dhidi ya mradi huo ulivyoandaliwa na kufanya kazi na namna ulivyopangiliwa kwa ustadi mkubwa.

Katika ziara hiyo inayotarajia kumalizika Machi 19, mwaka huu. Madiwani hao wakiongozwa na Mstahiki Meya wa Manispaaa ya Lindi, Frank Magali alipongea juhudi za UTT-PID kwa kufanikisha ziara hiyo kwani wamejifunza mengi na pindi watakaporejea Lindi, watakuwa mfano wa kuigwa.

“Kule kwetu Lindi pia tuna mradi uliopo katika hatua mbaali mbali na UTT-PID tayari wamesha pima baadhi ya viwanja katika mfumo kama huu wa kisasa tunaojifunza hapa hivyo itatusaidia sana kwa sasa” alisema Meya Magali.
Diwani wa Kata ya Nachingwea, Manispaa ya Lindi, Omari Chitanda akielezea namna alivyojifunza kwenye mradi huo kwa wandishi wa habari (hawapo pichani)
Diwani wa Kata ya Nachingwea, Manispaa ya Lindi, Omari Chitanda akielezea namna alivyojifunza kwenye mradi huo kwa wandishi wa habari (hawapo pichani).

Kwa upande wake, Diwani wa Nachingwea, Omari Chitanda alieleza kuwa, wamepata kuielewa vyema UTT-PID na naamna ya ufanyaji wake wa kazi.

“tunaipongeza UTT-PID kwani imetufungulia mwangaza wa kimaendeleo. Tutakapo rejea Lindi tutaenda kufanya mambo ya kimaendeleo katika kuubadilisha mji wetu” alisema Diwani Chitanda.
Aidha kwa upande wake msimamizi wa mradi huo wa Mapinga kutoka UTT-PID, Godfrey Charles alisema kuwa hdi sasa mradi huo umefanikiwa kwa kiwango ambapo tayari vimebaki viwanja vichache kati ya zaidi ya 500 vilivyochukuliwa.
Madiwani na maofisa kutoka UTT-PID wakifuatilia kwa makini maelezo ya msimamiz wa mradi huo wa Mapinga uliochini ya UTT-PID (Hayupo pichani
Madiwani na maofisa kutoka UTT-PID wakifuatilia kwa makini maelezo ya msimamizi wa mradi huo wa Mapinga uliochini ya UTT-PID (Hayupo pichani).

Pia madiwani hao, walipata elimu pamoja na ufanyaji wa kazi wa UTT-PID na wadau wanaoshirikiana nao huku hadi sasa ikiwa inasimamia miradi mbalimbali ikiwemo mikoa ya Pwani, Morogoro, Kagera, Dar es Salaam, Lindi na mikoa mingine hapa Nchini.

Aidha, kwa upande wa Madiwani hao walipongeza UTT-PID kwa hatua hiyo ya kuwapa elimu sambamba na kutembelea baadhi ya miradi inayoendeeshwa na taaisis hiyo.
..
New Mapinga Satellite town located 30km from Mwenge along new Bagamoyo road with hundreds of serviced plots for residential, commercial and trade purpose ready for sale. The town is fully installed with electrical, water and roads facilities.
DSCN9635
DSCN9651
DSCN9663
madiwani wa Lindi wakijadili jambo
Madiwani wa Lindi wakijadili jambo.

No comments: