Mkurugenzi
mkuu wa Airtel Tanzania Sunil Colaso akiongea na vijana 13 waliowezeshwa na
Airtel kupitia mradi wake wa Airtel FURSA walipotembelea ofisi za Airtel jijini
Dar es Salaam na kupata mafunzo ya kuendeleza biashara zao mwishoni mwa wiki
hii.Akishuhudia ni Mkurugenzi wa mawasiliano wa Airtel Beatrice Singano
(katikati) and (kushoto) Meneja huduma kwa jamii Hawa Bayumi.
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx
DAR ES SALAAM
Kampuni ya simu za mikononi ya Airtel kwa kupitia mradi wake wa
Airtel FURSA imewakaribisha vijana wajasiriamali 13 katika Makao makuu
yake yaliyopo Morocco na kujifunza uendeshwaji wa shughuli zake na kupatiwa
mafunzo zaidi ya kibiashara kwa muda wa siku tatu mwishoni mwa wiki iliyopita.
Meneja uhusiana na huduma kwa jamii wa Airtel Tanzania, Hawa
Bayumi akizungumzia hilo alisema, “Airtel kwa kupitia mradi wake wa Airtel
FURSA imeendelea kuwa mstari wa mbele kushirikiana na vijana katika kutatua
changamoto wanazozipata katika kujikwamua kiuchumi.
Alisema, “Tunayofuraha kuwakaribisha vijana wetu 13 tuliowawezesha
katika biashara zao na kujikwamua kiuchumi kwa kuwapa nyenzo za kisasa
zinazosaidia kukuza biashara zao na kujiongezea mapato. Pia ndani ya siku tatu
wameweza kupatiwa mafunzo zaidi yatakayo wafanya waweze kuendesha biashara zao
kwa njia ya kisasa na kuona ni jinsi gani wanaweza kuboresha biashara zao”.
Pia walifanikiwa kukutana na Meneja wa Airtel Tanzania Bwana.
Sunil Colaso na kumuelezea mafanikio waliyopata katokana na kuwezeshwa na
Airtel FURSA.
Bwana Sunil Colaso aliwaasa kutumia nafasi waliopata kujiendeleza
katika biashara zao na Airtel iko pamoja na vijana ili kuhakikisha malengo yao
yanatimia.
Iddi Chilumba mwakilishi wa vijana hao alisema, “Airtel FURSA
ilinikuta nikiwa na nauwezo wa kubanjua korosho chache kutokana na vifaa duni,
ila toka nimewezeshwa kwa mashine za kisasa na usafiri, sasa nabanjua korosho
nyingi na kusafirisha kwenye masoko mbalimbali kwa haraka Zaidi. Nawashukuru
sana Airtel kwa fursa walionipa na nawahasa vijana wenzangu wajishughulishe
kuliko kukaa kijiweni na kujishughulisha na vitendo viovu”.
“Tunafurahishwa sana na juhudi zinazofanywa na vijana
za kujitafutia maendeleo kwa njia zilizo halali na tuko tayari kushirikiana
nanyi katika kutatua changamoto mnazozipata kwa kupitia mradi wa Airtel FURSA”
alisema bwana Sunil Colaso.
No comments:
Post a Comment