Tangazo

October 31, 2015

SAID NA SALMA WALIVYOMEREMETA USIKU WA MAGUFULI

 Bwana Harusi Said akimnywesha Shampein mkewe Salma wakati wa sherehe ya ndoa yao iliyofanyika kwenye Uukumbi wa Best Choice uliopo Tabata jijini Dar es Salaam, jana usiku ambapo wanandoa hao walijiwekea historia ya ndoa yao kwa kusherehekea siku maalum ya utambulisho wa Rais mpya wa awamu ya tano Dkt. John Pombe Magufuli aliyekabidhiwa hati ya utambulisho wa ama cheti cha ushindi kwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania baada ya kuibuka kidedea katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu uliomalizika wiki iliyopita.

Aidha wanandoa hao walifunga Ndoa Okt 27 huko Karatu mkoani Arusha.
 Bi Harusi Salma akimlisha Keki mumewe Said ikiwa ni ishara ya upendo.
 Bwana harusi na Bi Harusi,wakimkabidhi keki Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi ya sherehe yao, George John, ikiwa ni sehemu ya kumshukuru kwa kusheresha na kufanikisha sherehe hiyo.
 Mdogo wa Bi harusi akifanya yake ukumbini hapo...
 Bw na Bi Harusi wakiwa katika pozi.... KUSOMA ZAIDI BOFYA READ MORE

 Baadaye ilikuwa ni mwendo wa Kwaito kama hivi.....
Baadhi wakishow love na maharusi....
 Kamati ikisonga kukabidhi zawadi kwa maharusi....
 Sebene la zawadi....
 Picha ya pamoja na wanakamati....
 Maneno ya shukrani.....
 Msanii wa muziki wa Injili, Mbasha, ambaye ni rafiki wa karibu na Bwana Harusi, akizungumza wakati wa sherehe hiyo, ambapo alimalizia na CCM oyeeeeeeeeeeeee, ukumbi ukaripuka oyeeeeeee
 Baada ya kuwapagawisha baadhi walishindwa kujizuia na kutoa skafu zao kibindoni na kumkabidhi mbasha kwa furaha......
 Msema chochote Mc, akimhoji mmoja wa wageni aliyefika kutoa zawadi maalum kwa maharusi..
 Mkono wa pongezi....
 Kamati kwa pamoja na maharusi.....
 Mama Mafoto akipata matukio ukumbini hapo....
Mwisho wa siku ilikuwa na Twist kama hivi ama veeeeeepeeeeee.....
. Picha na www.sufianimafoto.com

No comments: