Tangazo

August 31, 2016

AIRTEL NA VETA KUENDELEA KUELIMISHA VIJANA KUPITIA VSOMO APPLICATION



Afisa Uhusiano na matukio wa Airtel Tanzania, Dangio Kaniki akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya mafanikio ya mafunzo ya stadi za ufundi yanayotolewa na VETA kupitia mtandao wa simu ya mkononi wa Airtel yajulikanayo kama “VSOMO” yaani VETA SOMO katika ofisi za makao makuu ya Airtel Tanzania zilizoko Moroco jijini Dar es Saalam hapo jana.
XXXXXXXXXXXXXXXXXXXX 

DAR ES SALAAM 

Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel kupitia mpango wake wa kijamii wa Airtel FURSA ikishirikiana na  Mamlaka ya elimu ya ufundi Tanzania (VETA) imeendelea kuwawezesha vijana kupata kozi mbalimbali zinazotolewa katika vituo vya VETA nchini kupitia application ijulikanayo kama “VSOMO”  yaani VETA SOMO.

Akiongea na waandishi habari afisa Uhusiano wa Airtel Dangio Kaniki alisema, “vijana wameufurahia sana mpango huu unaowawezesha kusoma masomo kutoka VETA kwa urahisi zaidi na kuchochea kukua kwa elimu kwa vijana wengi na kuwawezesha kupata ujuzi wa ufundi na biashara itakayoongeza ufanisi wao.”

“Mafunzo kwa njia ya mtandao ni rahisi  na yatapatikana kwa wateja wa Airtel wenye simu zenye mfumo wa android.  Mteja atatakiwa kupakua application ya VSOMO kwenye orodha ya menu yake ya simu sehemu ya google play store na kujiandikisha bure.  Mara baada ya kumaliza masomo yake kwa 40% mwanafunzi atatakiwa kwenda kwenye kituo cha VETA kilichopo karibu nae na kujiandikisha kwaajili ya mafunzo kwa vitendo ambayo yatachukua muda wa wiki 2 kumaliza ikiwa ni sawa na masaa 60  na ndipo atakapokaa kwaajili ya mtihani na kutakiwa kufaulu kwa 60% “alisisitiza Kaniki.

Aliendelea kusema kuwa “vijana zaidi ya 19000 wamejisajili kusoma kozi mbalimbali kutoka VETA kupitia simu zao za mkononi. Kwasasa masomo yanayopatikana ni Ufundi pikipiki (bodaboda), Ufundi umeme wa manyumbani, Ufundi wa simu za mkononi, Ufundi Alluminium, utaalamu wa maswala ya urembo na ufundi wa kuchomelea vyuma.” 

Akibainisha hayo Kijana Saleh Shomari anayesoma kozi ya ufundi umeme  kupitia application ya VSOMO alisema “ VSOMO imekuwa msaada kwangu maana nilikuwa natamani kusoma kozi VETA lakini sikuwa na mda wa kufika chuo cha VETA kutokana na mihangaiko ya biashara zangu, lakini nawashukuru Airtel na VETA kulionahili na sasa najisomea mafunzo haya ya umeme jioni nikishafunga biashara yangu na kuweza kufikia malendo yangu ya kupata cheti kutoka VETA.”

Dangio alimalizia akisema” Mwanafunzi atatahiniwa na kisha kuandikishwa na kutakiwa kulipia kiasi shilingi 120,000/= kwa kupitia Airtel Money kwa kupiga *150*60# kama gharama ya mafunzo hayo. Tunatoa wito kwa vijana kutumia fursa hii ya kipekee ili kupata mafunzo ya ufundi kwa urahisi na gharama nafuu kwani gharama ya masomo iko chini zaidi.”

No comments: