Tangazo

August 24, 2016

RAIS DK. MAGUFULI AMUAPISHA BOSS MPYA WA USALAMA WA TAIFA

Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa, Dkt. Modestus Francis Kapilimba.
Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Rais Dkt. John Pombe magufuli akimuapisha Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa Dkt Modestus Francis Kapilimba Ikulu jijini Dar es salaam leo Agosti 24, 2016.


Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Rais Dkt. John Pombe Magufuli akimsikiliza  Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa Dkt Modestus Francis Kapilimba akila kiapo cha maadili ya viongozi wa Umma Ikulu jijini Dar es salaam leo Agosti 24, 2016. Kushoto akisimamia zoezi hilp ni   Kamishina wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Jaji Mstaafu Salome Kaganda.
Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Rais Dkt. John Pombe magufuli na Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan pamoja na  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Utumishi na Utawala Bora Mhe. Angellah J. Kairuki, Mwanasheria Mkuu wa  Serikali Mhe George Masaju na Katibu Mkuu kiongozi Engineer John Kijazi katika picha ya pamoja na viongozi wa vyombo vya ulinzi na usalama baada ya kuapishwa kwa  Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa Dkt Modestus Francis Kapilimba  Ikulu jijini Dar es salaam leo Agosti 24, 2016.
Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Rais Dkt.John Pombe magufuli katika picha ya pamoja na viongozi wa vyombo vya ulinzi na usalama baada ya kuapishwa kwa  Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa Dkt Modestus Francis Kapilimba  Ikulu jijini Dar es salaam leo Agosti 24, 2016. PICHA NA IKULU

No comments: