Tangazo

December 7, 2016

BancABC yatoa ofa kabambe

Mkuu wa Masoko na Hazina wa BancABC, Barton Mwasamengo, (kushoto), na Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi na wafanyabiashara wadogowadogo, Joyce Malai, wakionyesha kadi inayoonyesha uzinduzi wa ofa ya riba asilimia 16% kwa wateja wanaofungua akaunti ya amana ya muda maalum msimu huu wa sikukuu, katika hafla ya uzinduzi iliyofanyika katika  makao makuu ya BancABC jijini Dar es Salaam.

XXXXXXXXXXXXXXXXX
DAR ES SALAAM

BancABC yatoa ofa kabambe ya riba hadi 16% kwa wateja wanaofunga akaunti ya amana ya muda maalumu msimu huu wa sikukuu.

Benki ya ABC ambayo ni sehemu ya Atlas Mara imekuja na ofa maalumu kwa ajili ya wateja msimu wa sikukuu, ambapo wateja watakao fungua akaunti ya amana na kuweka pesa kuanzia milioni 10 kwa muda maalum atafaidika na ofa hii yakupata riba ya juu kuliko zote. 

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Mkuu wa kitengo cha wateja binafsi na wafanya biashara wadogo wa Benki ya ABC Bi Joyce Malai alisema tunaatoa riba ya hadi 16% kwa mwaka na kwamba watalipwa riba papo kwa papo ikiwa ni zawadi yao msimu huu wa sikuku.

“Hii ni ofa bora kuliko zote kwenye soko kwa sasa na tunataka kuwashawishi wateja wetu na hata wale wasiokuwa na akaunti kwetu kutumia fursa ya ofa hii ya msimu huu wa sikukuu,” alisema.

Mkuu wa  Idara hiyo ya Benki ya ABC alisema wana nia ya kufikia mahitaji ya wateja na kuhakikisha kwamba wanakua pamoja na benki hiyo. “Tunathamini jinsi wateja wetu wanavyotuunga mkono na hiyo ndio sababu sisi kama benki tumeamua kuwazawadia ofa hii kabambe katika msimu huu wa sikukuu,” alisema.

“Kinachotakiwa kufanywa na mteja yeyote ili aweze kujipatia ofa hii nikufika kwenye tawi letu lolote – Uhuru, Quality Centre, Kariakoo na Arusha, afungue akaunti ya amana ya muda maalumu ambapo riba hiyo italipwa papo hapo, lengo ni kukupa uhuru wa kuitumia kwa ajili ya kufanya manunuzi  binafsi kama upendavyo ikiwemo kununua zawadi kwa familia au marafiki ili kuwaongezea furaha katika msimu huu wa sikukuu,” alisema.

Aliendelea kusema kwamba ofa hiyo itawahusu wateja watakaofungua akaunti za amana za muda maalumu na Benki ya ABC Kabla ya Desemba 31, ikimaanisha kwamba ofa hiyo itakuwa halali kwa msimu wa sikukuu tu.

“Tunataka msimu huu wa sikukuu kuwa mzuri zaidi kwa wateja wetu kwa kuwa tunafahamu kwamba watu wengi hutumia kiasi kikubwa cha fedha wakati wa Krismasi. Kupitia riba hii watakayopata awali, wataweza kupata mahitaji yao kirahisi,” alisema.

No comments: