Tangazo

December 15, 2017

SBL yazindua kampeni ya kuitangaza Whisky ya Johnnie Walker Black Label



Mkurugenzi wa Masoko wa SBL Cesear Mloka Akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) mapema jana katika uzinduzi wa kampeni ya kuitangaza Whisky ya Johnie Walker Black label ambayo inaambatana na maadhimisho ya miaka 20 ya Kampuni mama ya Diageo.Pembeni yake ni Meneja Masoko  Nicholaus Machugu.



wadau wakionja ladha ya Whisky ya Johnnie Walker Black Label  mara baada ya uzinduzi wa kampeni ya kuitangaza mapema jana .

Mkurugenzi wa Masoko wa SBL Cesear Mloka Akizungumza na waandishi wa habari mapema jana katika uzinduzi wa kampeni ya kuitangaza Whisky ya Johnie Walker Black label ambayo inaambatana na maadhimisho ya miaka 20 ya Kampuni mama ya Diageo.

Ni katika kuadhimisha miaka 20 ya Kampuni mama ya Diageo

Dar es Salaam 

Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) leo imetangaza uzinduzi wa kampeni kwa ajili ya pombe kali aina ya Johnnie Walker (JW) Black Label inayojulikana kama, ‘JW Paints Tanzania Black’.

Katika kampeni hii, shughuli mbali mbali zitafanyika ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 20 ya kampuni mama ya Diageo yatakayofanyika tarehe 15/12/2017. Diageo ndiyo mwana hisa mkubwa kwenye kampuni ya SBL.

Ikiwa inatengenezwa na kampuni ya Diageo na kusambazwa na SBL kwa hapa Tanzania, Johnnie Walker Black Label ambayo ni Whisky ya Kiskoti inachukuliwa na wataalamu kama ndiyo whisky bora zaidi duniani huku ikijali thamani ya pesa kwa watumiaji wake.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Masoko wa SBL Cesear Mloka, kampeni hiyo itaanza kwa programu ya kuongezewa maarifa kwa wafanyakazi wa SBL ambayo itakwenda hadi katika ngazi ya marafiki, wanafamilia pamoja na wadau wa biashara.

“Tunatarajia kuwa na tukio la kufurahisha litakaloongozwa na wafanyakazi wetu ambao wataelezea ufahamu wao pamoja na mapenzi yao kwa Johnnie Walker kwa watumiaji wa kinywaji hicho kwenye sehemu mbali mbali kinapouzwa hapa nchini kama Bella Whispes, The Great, KB Tabata,Green Palm, Lachaz, MK, TIPS, Kuringe, Triple A, Front View, Dodoma Carnival na Golden Crest.

Tukio hili halitafanyika hapa Tanzania peke yake, bali linafanyika siku hiyo hiyo katika nchi 180 ambako Diageo inafanya biashara zake na ambako Johnnie Walker Black Label inapatikana. Tanzania ni sehemu  ya kampeni ya kidunia ya JW inayojulikana kama ‘Paint the World Black’ kuadhimisha shughuli hii yenye mafanikio makubwa,” alisema Mloka wakati wa uzinduzi uliofanyika Dar es Salaam.

Mloka aliongeza kuwa, kampeni hiyo itatangazwa kwenye magazeti, radio na televisheni, mitandao ya kijamii pamoja na vyombo vya mawasiliano ya ndani ya kampuni.

Kampuni ya SBL pia imezindua maeneo maalum ya kufanya manunuzi ya whisky ya Johnnie Walker Black Label mpaka mwishoni mwa mwezi Disemba katika maduka ya vileo yaliyopo Dar es Salaam ya Kibong'oto, Lamana, Master Liquor, Madeira & Herera pamoja na Arusha ya New Open Center & Chware Stores. Johnnie Walker Black Label iliyoyachanganywa ina umri wa miaka 12 na Ilitengenezwa wakati Johnnie Walker ikitimiza miaka 100 tangu ilipotengenezwa kwa mara ya kwanza mwaka 1909. Ladha yake ni mchanganyiko wa kipekee wa kimea, matunda, cocoa pamoja na vanilla.

Ikiwa inauzwa takribani kila nchi duniani, ni whisky ya Kiskoti inayosambazwa zaidi duniani.

JW Black Label inakuja katika kifungashio tofauti na endelevu (ikiwa kimstatili na nembo mbinjuko) huku ikitoa fursa maridhawa nay a hali ya juu ya ufungashaji wa zawadi kwa wale watumiaji wanaotazamia suluhisho la ufungashaji wa zawadi.

No comments: