Tangazo

March 21, 2018

MAWAKALA WA TIGO PESA NCHI NZIMA WAENDELEA KUJISHINDIA ZAWADI

Mkurugenzi wa Kampuni ya Mawasiliano ya Simu za Mkononi ya Tigo ,Kanda ya Kaskazin,Henry Kinabo akimkabidhi wakala wa Tigo Moshi mjini ,Hassan ,mfano wa Hundi ya Shilingi Milioni Mbili kwa kuibuka mshindi wa pili wa Promosheni ya Mawakala wa Tigo kwa kanda ya Kaskazini. Promosheni hii inawahusu Mawakala zaidi ya 73000 wa Tigo Pesa nchi nzima huku zawadi za Shilingi za kitanzania Milioni 144 zikishindaniwa. 

Mkurugenzi wa Kampuni ya Mawasiliano ya Simu za Mkononi ya Tigo ,Kanda ya Kaskazin,Henry Kinabo akimkabidhi wakala wa Tigo wilaya ya Same Real Stationary ,mfano wa Hundi ya Shilingi Milioni tatu  kwa kuibuka mshindi wa kwanza wa Promosheni ya Mawakala wa Tigo kwa kanda ya Kaskazini. Promosheni hii inawahusu Mawakala zaidi ya 73000 wa Tigo Pesa nchi nzima huku zawadi za Shilingi za kitanzania Milioni 144 
zikishindaniwa. 

Meneja wa Tigo Kanda ya Ziwa, Gwamaka Mwakilembe (kulia) akikabidhi mfano wa hundi ya shilingi milioni ,mbili kwa Juliana Shilatu aliyeibuka kama wakala wa pili bora wa kanda ya Ziwa katika promosheni ya mawakala wa Tigo Pesa. Zawadi zenye thamani ya TZS 88 milioni zimetolewa na Tigo pesa kwa mawakala wake 73,000 nchini kote walioshiriki katika promosheni hiyo.

Meneja wa Tigo Mkoa Iringa Davis Kisamo (kushoto) akimkabidhi mfano wa hundi ya shilingi millioni 3/- kwa wakala wa Tigo Pesa, Gibson Chaula wa Songea mwishoni mwa wiki mkoani Iringa.

Meneja wa Tigo Mkoa Iringa Davis Kisamo (kushoto) na Meneja Mauzo wa Tigo Mkoa Iringa, Samuel Chanay (kulia) wakimkabidhi mfano wa hundi wakala wa Tigo pesa Asha Ramadhani aliyeshindia zawadi ya shilingi millioni 2/-  kwenye hafla iliyofanyika mkoani Iringa mwishoni mwa wiki iliyopita.

No comments: