Tangazo

April 11, 2018

SERIKALI YAWAONYA WAFANYABIASHARA WA BIDHAA ZA MAGENDO MKOANI TANGA




MKUU wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa akizungumza wakati wa ufunguzi wa sherehe za wiki ya bandari pamoja na maadhimishi miaka 13 ya Mamlaka hiyo kulia ni Meneja wa Bandari ya Tanga Percival Salama kushoto ni Katibu Tawala wa wilaya ya Tanga Faidha Salim




Meneja wa Bandari ya Tanga Percival Salama akizungumza wakati wa ufunguzi wa sherehe za wiki ya bandari pamoja na maadhimishi miaka 13 ya Mamlaka hiyo kulia Afisa Mtekelezaji Mkuu wa Bandari ya Tanga Donald Ngaire kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa



PRO wa Bandari ya Tanga Moni Jarufu akizungumza wakati akiwakaribisha wageni kwenye sherehe hizo zilizofanyika kwenye viwanja v ya Bandari Jijini Tanga


Meneja wa Bandari ya Tanga Percival Salama katikati akifuatilia matukio mbalimbali kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa kulia ni Afisa Mtekelezaji Mkuu wa Bandari ya Tanga Donald Ngaire
Afisa Tehama wa Bandari ya Tanga Ally Isaka akimueleza kitu Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye sherehe hizo katikati ni Meneja wa Bandari ya Tanga Percival Salama
Meneja wa Bandari ya Tanga Percival Salama kushoto akiteta jambo na Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa mara baada ya kuwasili kwenye viwanja vya Bandari leo akiwa ameambatana na Mkuu wa Polisi wilaya ya Tanga (OCD) Jumanne Abdallah na Katibu Tawala wa wilaya ya Tanga Faidha Salim
Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa akisalimiana na wafanyakazi wa Bandari ya Tanga

Sehemu ya wafanyakazi wa Bandari ya Tanga wakimsikiliza Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa
Sehemu ya wafanyakazi wa Bandari ya Tanga wakimsikiliza Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa

Zoezi la utoaji wa damu likiendelea kwenye sherehe hizo

SERIKALI mkoani Tanga imesema kuwa haitakuwa na simile na wananchi watakaokamatwa kujihusisha na kuingiza bidhaa za magendo kupitia bandari bubu kwani wanachangia kuikosesha mapato serikali.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa wakati wa ufunguzi wa sherehe za wiki ya bandari pamoja na maadhimishi miaka 13 ya Mamlaka hiyo.

Alisema kuwa kumekuwepo na wimbi kubwa la wafanyabiashara wasio waaminifu kutumia bandari bubu kupitishia bidhaa za magendo ambazo sio salama kwa matumizi ya binadamu.

“Katika hili hatutakiwa na msamaha wala kumuonea mtu haya tukikukamata chombo tutakitaifisha pamoja na mali zake huku muhusika atachukuliwa hatua kali za kisheri nilazima wananchi wajifunzi kuona umuhimu wa kutumia bandari rasmi”alisema DC Mwilapwa.

Aidha aliitaka Mamlaka ya usimamizi wa bandari Mkoani Tanga kuhakikisha utendaji kazi wao unaendana na kasi ya maboresho ya bandari hiyo unaofanywa na serikali kwa sasa.

Awali Meneja wa Bandari ya Tanga Percival Salama alisema kuwa maboresho ya vifaa na vitendea kazi katika bandari hiyo yameweza kusaidia kuongeza ufanisi wa kuhudumia shehena za mizigo kutoka siku kumi hadi nne.

Alisema kuwa kuhudumia shehena za mizigo katika kipindi kifupi kumesaidia kupunguza gharama kwa wateja wanaohudumiwa na bandari hiyo . “Licha ya kuhudumia mizigo kwa awamu mbili lakini uwepo wa vifaa umesaidia kuboresha uwezo wa bandari yetu ya kuhudumia mizigo kwa ufanisi zaidi”alibainisha Mkuu huyo.

Sherehe hizo zinakwenda sambamba na kauli mbiu Bandari za TPA ni chachu ya uchumi Viwanda na Ustawi nchini Tanzania (Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha)

No comments: