Tangazo

February 21, 2012

NHIF WAZINDUA MRADI WA KUSAIDIA MAMA WAJAWAZITO NA WATOTO WACHANGA MKOANI TANGA

Mkuu wa Mkoa wa Tanga Chiku Galawa (kulia), akiteta jambo na Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, Imanuel Humba kabla ya uzinduzi wa mradi wa kusaidia mama wajawazito na watoto wachanga ambao upo chini ya usimamizi wa NHIF kwa Mikoa ya Tanga na Mbeya kwa majaribio.  Kushoto ni Mwakilishi wa KFW, Dk Kai Gesing.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga Chiku Galawa akikata utepe kuashiria uzinduzi wa mradi  wa kuwasaidia kupata huduma bora kwa mama wajawazito  na watoto walio chini ya umri wa miaka 5, hususani maeneo ya vijijini.

Mmoja wa wanufaika wa mradi KfW, akipokea kitambulisho cha kupata huduma za afya kwa niaba ya wenzake 600 kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga Bi Chiku Galawa,wanaoshuhudia pemben kulia ni Mkurugenzi mkuu wa NHIF, Imanuel Humba na Dr. Sweya ambaye ni Meneja wa Mradi kutoka NHIF.

Naibu Mkurugenzi Mkuu, Hamis Mdee akiteta jambo na Mkurugenzi Mkuu kuhusu namna ambavyo mradi huo unavyotekelezeka kwa kasi Mkoani Tanga kabla ya kuanza kwa mkutano wa uzinduzi.

Akina mama wajawazito waliowawakilisha wenzao 600 wakati wa kupokea vitambulisho vya huduma za afya wakiwa kwenye picha ya pamoja na wafadhili wa mradi (kfW)  na NHIF.

No comments: