Tangazo

May 24, 2012

MAJAMBAZI YAUA ASKARI POLISI KIGOMA


Na Pardon Mbwate na Felister Chubwa wa Jeshi la Polisi Kigoma

Askari Polisi mmoja mkoani Kigoma mwenye namba D.1645 Stafu Sajenti S/SGT George Luzegama(53), ameuwa kwa kupigwa risasi na majambazi.

Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Kigoma SSP Francis Mwakabana, amesema kuwa tukio hilo lilitokea jana majira ya saa 3.30 usiku huko kwenye eneo la Mwanga Kitambwe mjini Kigoma ambapo majambazi yakiwa na sihala aina ya short Gun walimpiga risasi askari huyo mwenye namba D.1645 S/SGT George Luzegama(53).

Kamanda Mwaakabana amesema askari huyo alipigwa risasi kwenye mbavu za upande wa kushoto alipokuwa kwenye duka moja la madawa ambapo majambazi walikuwa wamevamia hapo na walimshambulia wakidhani ni miongoni mwa askari walioweka mtego wa kuwanasa.

Askari huyo alifariki muda mfupi mara baada ya kufikishwa wakiwa katika Hospitali ya Maweni mkoani Kigoma alipokuwa akipatiwa matibabu.

Katika tukio hilo, majambazi hayo yalipora kiasi cha fedha za mauzo kutoka kwenye duka hilo na baadaye walikimbia kutokomea pasikojulikana na Polisi inaendelea na msako dhidi ya majambazi hayo.

Katika tukio hilo, muuzaji wa duka hilo Bi. Rehema Gwimo(30), alinusurika na anaendelea kuisaidia Polisi katika upelelezi wa tukio hilo.

Huyo ni askari wa nne kufariki mkoani Kigoma katika kipindi kisichozidi miezi miwili ambapo askari wawili walifariki dunia kwa ajali ya pikipiki na mwingine kuuawa na majambazi wakati wa mapambano kwenye ziwa Tanganyika. 

KATIKA TUKIO LINGINE Katika tukio linguine, Jeshi la Polisi mkoani Kigoma linamsaka mwananfunzi mmoja wa kidato cha nne katika shule ya Sekondari ya Mwike mjini Kigoma Bi. Rehema Issa(22) ambaye ni mkazi wa eneo la Kamara kwa tuhuma za kujifungua na kukitumbukiza kichanga chake chooni.

Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani humo SSP Francis  Mwakabana, amesema kuwa kichanga hicho ambacho kiliokolewa na wanafunzi wa shule mmoja ya msingi kikiwa hai lakini kilifariki muda mfupi wakati kilipokuwa kikipelekwa Hospitalini kwa matibabu.

Kufuatia matukio hayo, Kaimu Kamanada wa Polisi mkoani kogoma ametoa wito kwa wananchi kuendelea kutoa taarifa za kuwafichua wahalifu ili wakamatwe na kukabili mkono wa sheria.

No comments: