Tangazo

June 27, 2014

REDD'S MISS CHANG'OMBE ZAWADI ZA WASHINDI ZATANGAZWA

 Mratibu wa Shindano la kumtafuta mrembo wa Redd's Miss Chang'ombe, Tom Chilala (katikati), akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, leo wakati wa kuitangaza zawadi za washindi. Kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Marie Stopes, Dk. Jophn Bosco na Ofisa Uhusiano  wa TV1, Mponjoli Katule. 
 Warembo wa shindano la Redd's Miss Chang'ombe wakiwa katika picha ya pamoja na wadhamini wa shindano hilo, wasanii watakaotoa burudani siku ya fainali. 
 Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Marie Stopes, Dk. Jophn Bosco akifafanua jambo wakati wa mkutano na waandishi wa habari leo.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Marie Stopes, Dk. Jophn Bosco akifafanua jambo wakati wa mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, leo.
 Ofisa Uhusiano  wa TV1, Mponjoli Katule (wa tatu kulia) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu udhamini wa TV1 katika shindano la Redd's Miss Chang'ombe.
Rapa wa bendi ya Ruvu Stars, Msafiri Diouf 'Sokoine' akighani wakati wa mkutano na waandishi wa habari.
Warembo wakiwa wamepozi kwa picha.

Na Mwandidhi Wetu

MNYANGE atakayevishwa taji la Redds Miss Temeke  2014 linalotarajia kufanyika Juni 27 mwaka huu katika  ukumbi wa TTC Chang'ombe anatarajia kujinyakuria  kitita cha sh. laki tano. 
Mshindi wa pili atajinyakulia laki tatu, mshindi wa tatu  laki mbili na washiriki wengine watapata kifuta jasho cha sh. 65,000.

 Mratibu wa shindano hilo Tom Chilala, alisema katika  shindano hilo anatarajia kumtoa mrembo atakafanikiwa  kutwaa taji la misi Tanzania mwaka huu hapo baadaye.

"Mwaka huu nina warembo wazuri na wenye vigezo vyote, naamini mwaka huu nitarudisha heshima yangu ya  kufanikiwa kutoa warembo kutoka Redd's Miss Temeke hadi Redd's Miss Tanzania," alisema.

 Alisema mwaka 2010 alifanikiwa kumtoa Genevieve Emmanuel, kutoka miss Temeke hadi miss Tanzania,  hivyo na kwa mwaka huu anaamini itakuwa hivyo kutokana na warembo alionao. 

Aidha shindano hilo litakarokuwa na washereheshaji kutoka bendi ya Ruvu Stars, Mchekeshaji Kitale pamoja na msanii anayetamba na kibao cha Basi Nenda Moshi Katena na wengine. Kiingilio katika shindano hilo kitakuwa ni sh. 20,000 kwa VIP na Elfu 10000 kawaida. 

Naye Mkurugenzi wa Marie Stoper John Bosco ambao ni wadhamini wa shindano hilo alisema wameamua kudhamini mashindano hayo kwa lengo la kuwaelimisha vijana kuhusiana na uzazi wa mpango.

Alisema hawataishia hapo wanaendelea kudhamini hadi miss Tanzania kutokana na kuona vijana hao wanaweza kuliwakilisha taifa."Katika sensa viijana ndio wameonekana kuwa na asilimia kubwa hivyo ni vizuri kuwa dhamini ili kuweza kujenga kizazi ambacho kimewezeshwa ambacho hakitaweza kuwa taifa tegemezi," alisema.

No comments: