Tangazo

March 20, 2012

MIKUTANO YA KAMPENI ZA CCM ARUMERU MASHARIKI JANA

Mkazi wa Kijiji cha Uwiro kata ya Ngarenanyuki, jimbo la Arumeru Mashariki, Elielisia Kaayao akibandika kwenye duka lake bango la mgombea ubunge wa jimbo hilo kwa tiketi ya CCM  Sioi Sumari, jana.
Mgombea wa CCM jimbo la Arumeru Mashariki, Sioi Sumari  akisalimiana na wananchi kwa bashasha alipowasili kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika eneo  la Olkung'wado kata ya Ngarenanyuki jimboni humo jana Machi 19.12.

Wananchi wa kijiji cha Ngabobo wakimthibitishia mratibu wa kampenbi za CCM uchaguzi mdogo jimbo la Arumeru Mashariki, Mwigulu Nchemba (kshoto) kuwa watampa kura mgombea wa CCM Sioi Sumari , wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika katika kijiji hicho, jana.

Mwigulu (kushoto) akiwa amejichanganya na wamasai kwenye mkutano wa Ngabobo, Ngarenanyuki wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika katika kijiji hicho juzi.


Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Steven Wasira akimnadi Sioi mkutano wa Uwiro, Ngarenanyuki.

Wazee na Kijana wakimsikiliza kwa makini mgombea wa CCM Sioi Sumari kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika jana kijiji cha Uwiro, kata ya Ngarenanyuka.

Sioi na mbunge wa Ngorongoro, Lekule Laiza wakizungumza jambo baada ya mkutano wa kampeni wa kijiji cha Uwiro, Ngarenanyuki. kulia ni Wasira.

Sioi akiwasalimia vijana  kijiji cha Uwiro, Ngarenanyuki baada ya mkutano wa kampeni.

Kina mama wa Ngabobo wakienda kwenye mkutano wa kampeni wa Sioi kwenye kijiji hicho.

Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM,  Asha Abdallah Juma akihutubia mkutano wa kampeni kijiji cha Olkung'wado.

Kina mama  wa Olkung'wado kata ya Ngarenanyuki wakimshangilia mgombea wa CCM, Sioi.

No comments: