Tangazo

November 29, 2014

AJALI YA HELKOPTA LEO; MARUBANI WA POLISI WAFARIKI

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadiki na Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, CP Suleiman Kova wakiwa eneo la ajali. Picha ndogo ni Mrakibu wa Polisi Capt. Kidai Senzala enzi za uhai wake.
Helkopta hiyo ilivyo haribika.
Wananchi wakiwa eneo la tukio. Kwa Hisani ya Father Kidevu
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

HELKOPTA ya wizaya ya Maliasili na Utalii iliyo tolewa msaada kutoka kwa Taasisi ya Howard G. Foundation inayomilikiwa na mfanyabiashara mashuhuri nchini Marekani Bw. Warren Buffet  na kupokelewa nchini na Waziri wa Maliasili na Utalii June 14, 2014 jijini Dar es Salaam imepata ajali na kuua watu wanne hii leo.

Helkopta aina ya Robertson R44 hiyo ambayo baade ilikabidhiwa kwa Mamlaka ya Hifadhi za Wanyamapori Tanzania (TANAPA) ilipata ajali majira ya saa nne asubuhi baada ya kupata hitlafu katika injili yake.

Mashuhuda walioshuhudia ajali hiyo eneo la Kipunguni B- Ukonga Moshi Bar Ilala Dar es Salaam waliambia Father Kidevu Blog kuwa awali waliona helkota hiyo ikiyumba na kutoa mngurumo usio wa kawaida na baade kuzima kisha kusikika kuwashwa bila mafaniko na baade kuanguka.

"Tulisikia mlio wa Helkopta usio wa kawaida, na baadae ulizima na kusikika tena kuwashwa ikagoma lakini tukasikia tu kishindo kikubwa cha Helkopta hiyo kuanguka," alisema shuhuda huyo.

Kamanda wa Polisi Viwanja vya Ndege, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Hamisi Seleman aliambia Father Kidevu Blog kuwa walio kufa ni Marubani wa tatu kati yao wawili ni marubani wa polisi na Afisa mmoja wa Polisi.

ACP Selemani aliwataja waliopoteza maisha kuwa ni Mrakibu wa Polisi Capt. Kidai Senzala Kaluse, Mkaguzi wa Polisi Capt. Simba Musa Simba,  Konstebo wa Polisi, Josso Selestine na Capt. Joseph Khalfan.

No comments: