xxxxxxx
Na Martha
Komba
Serikali
imeiagiza Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (CHRGG) kuibua masuala
yanayoathiri uzingatiaji wa haki za binadamu ili hatua stahiki zichukuliwe na
hivyo kuboresha misingi ya haki na utawala bora nchini.
Akizungumza
na viongozi wa Tume hiyo jana (Jumanne, Feb. 24, 2015) jijini Dar es Salaam,
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Asha–Rose Migiro alisema Serikali ina wajibu
wa kuzingatia haki za binadamu katika utekelezaji wa majukumu yake na hivyo na
hivyo ni muhimu kwa Tume kuibua na kutoa taarifa juu ya masuala ya ukiukwaji wa
haki za binadamu.
“Serikali
ina wajibu wa kufanya kazi kwa kuzingatia na kulinda haki za binadamu ili
wananchi waweze kuwa na amani katika nchi yao,” alisema Dkt. Migiro katika
mikutano wa viongozi wa Tume hiyo uliohudhuriwa Naibu Waziri wa Katiba na
Sheria Mhe. Ummy Mwalimu. Waziri Migiro alikuwa katika ziara ya kubadilishana
mawazo na uzoefu na viongozi wa Tume hiyo.
Tume
ya Haki za Binadamu na Utawala Bora ilianzishwa mwaka 2000 na kuanza kazi rasmi
mwaka 2002 ili, pamoja na majukumu mengine, kutoa ushauri kwa serikali na
vyombo vingine vya umma na vya sekta binafsi kuhusu haki za binadamu na utawala
bora.
Akizungumza
katika mkutano huo, Naibu Waziri alisema ni muhimu kwa Tume hiyo kuongeza kasi
ya kutoa elimu kwa umma kuhusu uzingatiaji wa haki za binadamu na utawala bora kwa
kutumia teknolojia ya habari na mawasiliano ili kuwafikia wananchi wengi kwa
kasi na haraka.
“Katika
nchi yetu suala la teknolojia ya mawasiliano na habari ni muhimu sana ili
kufikisha ujumbe kwa wananchi kwa kasi na kwa haraka zaidi, ongezeni kasi ya
kuitumia,” Naibu Waziri aliwaambia
viongozi hao walioongozwa na Mwenyekiti wa Tume hiyo Wakili Bahame Tom Nyanduga.
Kwa
upande, Mwenyekiti wa Tume hiyo aliwashukuru Waziri na Naibu Waziri kwa ziara
yao kwa Tume na kuahidi kutekeleza maelekezo waliyopewa pamoja na changamoto
zilizopo.
Aidha,
Wakili Nyanduga alisema kuwa Tume yake ina mpango wa kuandaa programu ya
kuelimisha umma juu ya watu wenye ulemavu wa ngozi kwa kuwa wao pia wana haki
ya kuishi.
“Kuwaua
watu wenye ulemavu wa ngozi ni ukiukwaji wa haki za binadamu kwa vile wao pia
wana haki ya kuishi,” alisisitiza Mwenyekiti huyo na kufafanua kuwa Tume
inaandaa mpango wa kuelimisha umma ili kukomesha mauaji hayo.
Pamoja
na Mwenyekiti wa Tume, mkutano huo ulihudhuriwa na Makamu Mwenyekiti Bw. Iddi Ramadhani Mapuri, Makamishna Tume hiyo
Bw. Mohammed Khamis Hamad, Dkt. Kevin Mandopi, Bi. Rehema Msabila Ntimizi, Bi.
Salma Ali Hassan, Katibu Mtendaji wa Tume Bi. Mary Massay na viongozi wengine
wa tume.
No comments:
Post a Comment