Tangazo

April 13, 2015

RAIS KIKWETE AZINDUA KOZI MAALUMU YA MAADILI NA UONGOZI, AMSIMIKA MZEE MSEKWA KUWA MWENYEKITI WA KIBWETA CHA MWALIMU NYERERE


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akizindua kitabu cha Programu ya Uongozi na Maadili  katika Chuo cha Kumbukumbu ya Nyerere Kigamoni jijini Dar es salaam leo. Kushoto kwake  ni Waziri wa Elimu Dkt Shukuru Kawambwa na kulia kwake ni Mkuu wa Chuo hicho Profesa Shadrack Mwakalila.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimsimika rasmi Mzee Pius Msekwa kuwa Mwenyekiti wa Kibweta cha Mwalimu Nyerere cha Uongozi na  Maadili wakati wa uzinduzi wa Kozi Maalum ya Maadili na Uongozi katika Chuo cha Kumbukumbu ya Nyerere Kigamoni jijini Dar es salaam leo.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimsikiliza  Mzee Pius Msekwa akitoa shukurani baada ya kusimikwa rasmi kuwa Mwenyekiti wa Kibweta cha Mwalimu Nyerere cha Uongozi na  Maadili wakati wa uzinduzi wa Kozi Maalum ya Maadili na Uongozi katika Chuo cha Kumbukumbu ya Nyerere Kigamoni jijini Dar es salaam leo. Kushoto kwake  ni Waziri wa Elimu Dkt Shukuru Kawambwa na kulia kwake ni Mkuu wa Chuo hicho Profesa Shadrack Mwakalila. PICHA NA IKULU

No comments: