Tangazo

April 14, 2015

TWANGA PEPETA KUWATAMBULISHA ALLY CHOKI NA SUPER NYAMWELA KATIKA KIOTA CHA ESCAPE ONE IJUMAA APRIL 24

 Ule utambulisho wa Ally Choki akiwa na Twanga Pepeta sasa ni Rasmi siku ya Ijumaa tarehe 24-04-2015.

- Utambulisho huo unafanyika Escape One Mikocheni.

- Utambulisho wa Ally Choki unaenda sambamba na Utambulisho wa Densa bora kabisa Super Nyamwela.

- Mazoezi ya utambulisho huo yameanza toka wiki iliyopita ambapo yanaenda pamoja na kutengeneza nyimbo tatu za Ally Choki ambazo ni "Kichwa Chini", "No Discussion" na "usiogope Maisha".

- Twanga kwa sasa inafanya mazoezi Kunduchi Salasala nyumbani kwa mdau mkubwa wa Twanga, Yusuphed Mhandeni na Mkewe Karima ChiChi Mhandeni. Saluti kubwa kwenu!!
 Stori kwa Hisani ya Jukwaa la Twanga Pepeta

No comments: