Tangazo

July 30, 2015

Airtel yazindua Duka jijini Tanga

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Said Magalula (katikati), akikata utepe kuzindua Duka jipya la Airtel Tanzania lililopo katika Barabara ya Uhuru jijini Tanga jana. Kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Huduma kwa Wateja wa Airtel, Adriana Lyamba na (kulia kwake) ni Afisa wa Huduma kwa Wateja wa Duka hilo, Mwanavita Chiya.
Mkurugenzi wa Huduma kwa Wateja wa Airtel, Adriana Lyamba (wa pili kushoto), akifafanua jambo kwa  Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Said Magalula (kushoto), kuhusu bidhaa mbalimbali zinazouzwa katika Duka jipya la Airtel Tanzania lililopo katika Barabara ya Uhuru jijini Tanga, baada ya mkuu huyo wa mkoa kuzindua duka hilo jana.
Mkurugenzi wa Huduma kwa Wateja wa Airtel, Adriana Lyamba (kushoto), akifafanua jambo kwa  Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Said Magalula (mwenye miwani), baada ya mkuu huyo kuzindua Duka jipya la Airtel Tanzania lililopo katika Barabara ya Uhuru jijini Tanga jana.
Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Said Magalula (wa pili kushoto), akikagua Duka jipya la Airtel Tanzania baada ya kulizindua katika hafla iliyofanyika dukani hapo katika Barabara ya Uhuru jijini Tanga jana. Kushoto ni Mkurugenzi wa Huduma kwa Wateja wa Airtel, Adriana Lyamba.


Mkuu wa Mkoa wa Tanga,  Said Magalula (kulia), akiwa na Mkurugenzi wa Huduma kwa Wateja wa Airtel, Adriana Lyamba baada ya mkuu huyo, kuzindua Duka jipya la Airtel Tanzania lililopo katika Barabara ya Uhuru jijini Tanga jana.
Xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel leo imezindua duka lake jipya katika mkoa wa Tanga ikiwa ni jitihada zake za kuhakikisha inawapatia wateja wake nchi nzima huduma bora na za kisasa.

Duka hilo la kisasa,  liko katika maeneo ya tanga mjini, Barabara ya Uhuru, kwenye jingo la nyumbani hoteli. Huduma zinazotolewa na duka hilo ni pamoja na kukusanya Ankara, kurudisha namba zilizopotea, mauzo ya simu hasa smartphone, Airtel money, kusajili namba pamoja na huduma za kimitandao.

Akiongea wakati wa uzinduzi , Mkurugenzi wa Kitengo cha huduma kwa wateja wa Airtel, bi Adriana Lyamba alisema” uzinduzi wa duka hili ni uthibitisho wa dhamira yetu ya kutoa huduma bora na kuwapatia  wateja wetu uzoefu toufati  katika huduma zetu.  Leo tunawawezesha wateja wetu na wakazi wa mkoa wa Tanga kupata hudumu muhimu kama vile za kifedha za Airtel Money kwa usalama zaidi pamoja na kuwaunganisha na simu za kisasa za smartphone na huduma zetu za intaneti”.

“Sambamba na hilo, duka letu pia litatoa ofa kabambe za simu na vifaa vya aina tofauti na kuwawezesha wateja wetu kunganishwa na tecknologia ya simu za mkononi ya kisasa Tunaamini vifaa vya kisasa ni sehemu muhimu ya mahitaji ya wateja wetu kwa sasa,  hivyo kupitia watoa huduma wetu waliobobea kwenye maswala ya tekinologia tunawewezesha wateja wetu kuchangua vifaa na simu bora pamoja na kuwaunganisha na huduma za intanet. Ni matumanini yangu kuwa wateja wetu sasa watapata suluhisho la mahitaji yao ya huduma za simu kwa urahisi kupitia duka hili.” Aliongeza Lyamba.

Akizindua duka hilo Mkuu wa Mkoa wa Tanga , Magalula Said Magalula alisema “Mawasiliano yanachangia kwa kiasi kikubwa katika kuwaunganisha watu na biashara na kukuza uchumi wa nchi. Nawapongeza Airtel kwa kuongeza wigo kupitia huduma kwa wateja na kuleta mabadiliko ya kibunifu. Tunaamini ubunifu huu utawawezesha wakazi waTanga kupata huduma bora wakati wote,  na kwa hilo Tunawashukuru sana Airtel. 

“Natoa wito kwa wakazi wa Tanga na wateja wa Airtel kutembelea duka hili  na kufurahia huduma na bidhaa za kisasa ikiwemo huduma ya Airtel Money inayotoa suluhisho kwa mahitaji yao ya huduma za kifedha, kufanya malipo na kutuma pesa kirahisi  zaidi” alisema Magalula.

Mkuu wa Mkoa aliwaasa makampuni mengi zaidi kuiga mfano wa Airtel katika kutoa huduma bora na kusema Serikali iko tayari kushirikiana nao katika kuhakikisha inaboresha maisha ya wakazi na watanzania wa ujumla katika maeneo mbalimbali nchini.

No comments: