Tangazo

April 1, 2016

JOKATE NA MO DEWJI FOUNDATION KUJENGA KIWANJA CHA MICHEZO SEKONDARI YA JANGWANI

Jokate
Mwanzilishi wa ujenzi huo, Jokate Mwegelo akiandika jambo wakati ujenzi wa kiwanja ukiendelea.

Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Jangwani wanataraji kunufaika kwa kupata uwanja wa michezo ambao unajegwa kwa ushirikiano wa Mwanamitindo Jokate Mwegelo na Taasisi ya Mo Dewji.

Akizungumza na Mo Blog, Jokate amesema ujenzi wa kiwanja hicho cha michezo ni sehemu ya mipango aliyokuwa nayo baada ya kuanzisha mwaka jana bonanza la Kidoti ambalo lilikuwa na malengo ya kuhamasisha wanafunzi kufanya vizuri kimasomo na kushiriki katika michezo ili kukuza vipaji vyao.

Jokate amesema ameamua kuanza na shule ya Jangwani kwa kutambua kuwa shule hiyo ina hosteli za wanafunzi walemavu na wamekuwa wakipata shida kupata viwanja vya michezo hivyo kupitia kiwanja hicho wataweza kushiriki michezo kwa urahisi zaidi.

“Pale Shule ya Jangwani kuna wanafunzi walio na ulemavu na kama unavyojua mlemavu anatakiwa kufanya mazoezi ili kuweka afya yake vizuri na kama wakitaka kushiriki michezo hadi waende Gymkhana lakini tunawajengea uwanja wa Basketball na Netball,” amesema Jokate wakati akifanya mahojiano na Mo Blog.

Ameongeza kuwa ili kufanikisha ujenzi huo alizungumza na Mohammed Dewji ambaye alikubali kutoa Milioni 10 kupitia Taasisi yake ya Mo Dewji na hivyo kuanza kufanyika kwa ujenzi huo ambao utawawezesha wanafunzi wa Jangwani kushiriki michezo tofauti na hapo awali.

Aidha amesema kuwa ujenzi wa viwanja vya michezo utakuwa endelevu katika shule za serikali ambazo bado hazijawa na viwanja na baada ya kukamilika kwa ujenzi katika shule ya Jangwani amepanga kufanya ujenzi wa viwanja vya michezo katika Shule ya Sekondari Kinyerezi na Shule ya Sekondari Maposeni iliyopo wilayani Peramiho, Ruvuma.
14581134867112
Ujenzi wa kiwanja cha michezo katika Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Jangwani ukiendelea
IMG_3708
IMG_3868
IMG_3869
IMG_3872
IMG_3875
IMG_3878
IMG_3883
IMG_3884
IMG_3880
Jokate Mwegelo akibadilishana mawazo na fundi anayejenga uwanja huo wa michezo.

No comments: