Tangazo

December 9, 2016

TAMASHA LA SIFA ZA YERIKO ARUSHA



Miaka 25 ijayo, Takribani asilimia 75 ya wakazi wa Afrika Mashariki watakuwa vijana,na hii inamaanisha nguvukazi kubwa itakuwa mikononi mwao. Lakini kama watasalia kuwa idadi kubwa basi na kuwa na maarifa ya kuendesha nchi, basi changamoto itakuwa kwa ukuaji wa nchi.

Vijana wao huona kama wana mchango katika jamii, hasa kwenye makusanyiko ya kijamii mathalani misiba, ambapo hutakiwa kuchangamkia kwenye shughuli zenye uhitaji wa nguvu. 

Lakini kama fursa ya uwepo wa vijana katika jamii itatumiwa vema, basi nyanja zote za maendeleo zitaendeshwa vema, na watakuwa na uwezo wa kutatuza matatizo yaliyo kwenye jamii – sawasawa na malengo endelevu namba 2 na namba 8 za umoja wa mataifa, zinazolenga kumaliza masuala ya njaa, na pia uhakika wa kazi na ukuaji wa uchumi, ikiwemo pia lengo namba 4 – kuwa na elimu bora.

Uwepo wa Tamasha la Sifa za Yeriko ni sehemu ya mkakati wa muda mrefu wa Maono Foundation Limited na washirika wake kuwa sehemu ya kutatua matatizo haya kwa kuanzisha kituo cha ukuzaji wa vipaji kwa vijana, kusudi waweze kuwa sehemu ya suluhu ya changamoto kwenye jamii.Mkakati wa muda mfupi, ni kuhudumia moja ya kituo cha watoto yatima cha Guardian Angels House of Hope chenye uhitaji wa taaluma za watoto kukuzwa,lakini changamoto ikawa kukosekana kwa ada na mahitaji mengine ya shuleni.

Kwa kujumuika kwenye tamasha hili, si tu kwamba watakuwa wanamuaibisha mwovu shetani kwa kuangusha ngome zinazowasumbua kwenye Nyanja mbalimbali maishani, bali pia watakuwa wamechangia katika kutimia kwa malengo ya Maono Foundation.

Tamasha la Sifa za Yeriko msimu wa kwanza inatarajiwa kufanyika tarehe 9 Disemba 2016 Jijini Arusha kwenye Kanisa la New Life City Church (Kwa Egon) lililoko Kwa Iddi, na kisha kufuatiwa na Tamasha la pili litakalofanyika tarehe 11 Disemba Kanisa la Tanzania Assemblies of God CCC Upanga Jijini Dar es Salaam ikiwa ni weekend hii. Tamasha hili litahusishwa waimbaji wa ndani na nje ya Tanzania, ambapo ugeni kutoka Afrika Kusini utakuwepo. 

Wageni hawa ni Mercy Manqele, KgotsoMakgalema na Sipokazi Nxumalo.Baadhi ya waimbaji wa ndani ni kama vile, Abednego na The Worshippers, Toddlers International, Yusuphu Nahashon, Kwaya ya Uinjilisti Kijitonyama,Wengine ni Machalii wa Yesu, The Cahogoz, Voice of Joy, Lilian Kimola, na Bomby Johnson.

LENGO

Lengo la awali nikukusanya kiasi cha shilingi milioni 200 ambazo zitatumika
kutafuta eneo la kituo kwa jijini Dar es Salaam na Arusha, pamoja na matengenezo iwapo itanunuliwa nyumba na kuibadilisha kuendana na maono ya jinsi kituo tunavyotaka kiwe kukidhi mambo mbalimbali yatakayokuwa yakipatikana kituoni, kama kujifunza muziki, uimbaji, ushauri nasaha, na utafutaji wa shule za kukuza vipaji ndani na nje ya nchi.ambayo tunatarajia yatawezesha kupatikana kwa kiasi hiki ni kupitia barua za mwaliko kwa watumishi mbalimbali wa dini na taasisi, pamoja na kiingilio kitakachopatikana kupitia matamasha yote mawili.

GHARAMA

Ili lengo la kukusanya milioni 200 kutimia, gharama mbalimbali kutoka kwa waanzilishi na marafiki zimefanikisha katika kuwakaribisha waimbaji hawa kutoka Afrika Kusini, kulipia mahala watakapofikia, matangazo, usafiri wa ndani, chakula, vyombo, muziki na gharama nyinginezo. Hili litasaidia katika ukusanyaji wa kiasi kilichosalia kwa awamu tofauti tofauti. Tunaamini katika ushirikiano katika kutatua matatizo yaliyomo kwenye jamii yetu

Katika Kufanikisha na maono ya kupata fedha katika Tamasha hilo kwa Dar es salaam na Arusha kutakuwa na Kiingilio katika Matamsha hayo,Arusha ni Ijumaa hii Dec 9 pale kwa Egon Wakubwa 5000 VIP 20000 Dar es salaam ni Jumapili hii Dec 11 pale CCC Upanga Opp Chuo cha Mzumbe Watoto 5000 Wakubwa 10000 VIP 30000


Tunategemea support yenu wadau wa vyombo vya habari Bloggers kwa kwa ajili ya kusaidia kutangaza Tamasha hili linalofanyika lengo na maono tuliyo nayo mbele yetu Arusha na Dar es salam kwa wikendi hii.

No comments: