Tangazo

January 4, 2017

WALEMAVU WA KIJIJI CHA LULANZI WAMLILIA MBUNGE RITTA KABATI

 Mbunge wa viti maalum mkoa waIringa(CCM) Rita Kabati akiongea na familia ya watu watano wenye ulemavu wa viungo alipowatembea katika kijiji cha Lulanzi kata ya Mtitu wilayani Kilolo mkoa wa Iringa wakati wa kuwasaidia msaada kukarabati nyumba yao pamoja na kuwapa vitu vingine vya kimsaada
Leah mwamoto mtoto wa mbunge wa jimbo la kilolo Vennance Mwamoto naye alishuhudia maisha magumu wanaoishi familia ya watu watano wenye ulemavu wa viungo alipowatembea katika kijiji cha Lulanzi kata ya Mtitu wilayani Kilolo mkoa wa Iringa na hapo aliposimama ndio choo kinachotumiwa na familia hiyo kwa sasa huku wakisubili ujenzi wa choo kipya kinachoendelea kujengwa kwa hisani ya mbunge Ritta kabati
 Hivi ni baadhi ya vifaa vilivyoletwa na mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa kupitia chama cha mapinduzi (CCM) Rita Kabati kwa ajili ya kuwasidia familia ya watu watano wenye ulemavu wa viungo alipowatembea katika kijiji cha Lulanzi kata ya Mtitu wilayani Kilolo mkoa wa Iringa

Na fredy mgunda,Iringa

FAMILIA ya watu watano wenye ulemavu wa viungo wamemuomba mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa kupitia chama cha mapinduzi (CCM) Rita Kabati kuendelea kuilea familia hiyo kama familia yake.

Akizungumza na blog hii mmoja wa wanafamilia hiyo,Elias Mpogole ambaye ni mlemavu alisema kuwa mbunge huyo amekuwa akiwasaidia toka siku ya kwanza walipokutana naye katika kijiji hicho cha Lulanzi.

“Zamani tulikuwa tunaishi kwenye nyumba ambayo inavuja haina dilisha wala mlango pia tulikuwa tunalala chini lakini mbunge Kabati katusaidia nyumba nzuri kama mnavyoiona waandishi,katuletea magodoro,mashuka,blanket na sasa ameanza kutujenga choo cha kisasa na ameshawalipa mafundi pesa zote ndio maana tunaomba anendelee kuwa na sisi.”Alisema Mpogole

Mpogole alishukuru msaada waliopatiwa na kuwataka wadau wengine waweze kujitokeza zaidi kuwasaidia kuwapatia vyakula na radio za kuwezakusikiliza nyimbo za dini.

Kwa upenda wake mbunge wa viti maalum mkoa waIringa(CCM) Rita Kabati ametoa msaada wa vitu mbalimbali ikiwemo ukarabati wanyumba kwa familia yenye watoto walemavu wanne wa kijiji cha Lulanzi kilichoko kata ya Mtitu wilayani Kilolo mkoa wa Iringa. 

Msaada huo wa ukarabati wa nyumba,umeambatana na magodoro, vyakula na ujenzi wa choo cha kisasa ameutoa baada yakuwahidi kufanyia matengenezo ya nyumba ambayo walikuwa wakipata shida kipindicha masika mara baada ya kufanya ziara mapema mwaka huu katika kijiji hicho nakugundua mateso wanayokumbana nayo familia hiyo. 

 "Nimeitembelea familia hiinimeumia sana kwani maisha wanayoishi ni ya shida sana hawana msaada wowotenyumba yao inavuja hawana chakula maishayao ni ya kuunganga unga mpaka watu  wajekama sisi kuwaletea vitu  vidogo vidogokama mchele na mafuta na mbaya Zaidi hata watoto hao wote watatu hakuna hatammoja aliyewahi kukanyaga shule ingawa wanaonekana ni wakubwa hivyo jamii tunapaswa kuwasaidia watoto hawa” alisema Kabati  

Familia hiyo ambayo baba mzazi Mzee LucasMpogole mbaye kwa sasa amelazwa hospitali ya mkoa wa Iringa kwa ugonjwa wakupooza ina watoto wanne wote wakiwa walemavu wa viungo hivyo kukosa msaadakabisa pindi mvua zikianza kijiji hapo. 

Akizungumza wakati wa kukabidhimsaada huo , Kabati alisema kuwa jamii ya walemavu wanahitaji msaada wa hali namali kutoka kwa wadau wenye uwezo na kuacha tabia ya kuiacha serikali peke yakekatika kutatua kero zao na kuwahudumia.

Alisema kuwa msaada huo utawafarijiwalemavu hao waone kuwa pamoja na upungufu walionao bado jamii ya watanzaniainawathamini na kuwajali katika maisha yao ya kila siku.

 Aliongeza kuwa walemavu wanayo hakiya kuishi na kujitegemea iwapo jamii itawajengea uwezo badala ya kuwafungiandani na kuwaona kama ni mkosi katika familia ila kugundua vipajiwalivyonavyo na kuiwezesha serikali kuwaingiza katika mipango mbalimbali yakuwapatia huduma. 

Kabati alitoa wito kwa serikalikuona umuhimu wa kutumia vituo mbalimbali vinavyolea watoto wenye ulemavukuhakikisha vinawejengea miundo mbinu rafiki na uboreshaji mipango na mfumo wautoaji elimu, afya na usafiri kulingana na tofauti za umri wa watoto nchini. Aidha Kabati alitoa wito kwa Mfukowa Maendeleo ya Jamii (TASAF) kuangalia kwa jicho la tatu familia ya Mpogolekwa kuwaongezea kipato zaidi cha kila mwezi kwani kwa hali waliyonayo nakiwango wanachopata kila baada ya miezi miwili hakiendani na uwingi wa walemavuwa familia hiyo maskini. 

Naye baba mdogo wa watoto hao akiongea kwa niaba ya baba mzazi wa walemavu hao, Juma Mpogole alimshukurumbunge huyo kwa msaada aliotoa na kumtaka awasomeshe watoto wake ambao tangu wazaliwe hawajawahi pata elimu yoyote licha ya kufikisha umri wa miaka zaidi 20.

Lakini naomba nitoe rai kwa wale wanasiasa na wananchi wengine wanaokuja kupiga picha nah ii familia ya watu wenye ulemavu wa viungo kwa ajili ya kujitafutia umaarufu waache tabia hiyo.

“Kila mara tunaona waandishi na wapiga picha wanafika hapa na viongozi mbalimbali lakini kila siku wanatoa ahadi tu sioni msaada wowote ule unaotolewa zaidi ya kuona wanajitafutia umaarufu huko mitaani naomba waacha tabia hiyo sisi tunamuona mbunge Ritta Kabati na kaka yake mbunge wa jimbo hili la kilolo Vennence mwamoto ndio wanaosaidia familia hii,kweli familia hii inaitaji msaada hivyo njooni kutoa msaada sio kupiga picha pekee yake”.alisema Mpogole

No comments: