Tangazo

June 9, 2017

Shania aachia 'Shirawadu'

NA MWANDISHI WETU

‘SHIRAWADU’ ni ngoma mpya kabisa ya mduara ambayo wiki hii imeachiwa rasmi kutoka kwa msanii anayekuja juu kwa kasi ya ajabu, Shania Kabeya.

Studio ya 442 Music iliyoko Karakata, Kipawa, jijini Dar es Salaam chini ya Mtayarishaji Tamimu Hamis ‘Mabanga’ ndipo ilipopikwa ngoma hiyo iliyobeba ujumbe mzito juu ya wapenzi anavyotakiwa kutoyafuatilia maneno ya watu wa pembeni.

Kwa upande wake Shania mwenyewe, hii ndio ngoma yake ya kwanza ambapo hata hivyo yuko mbioni kuandaa kazi nyingine ‘sumu’, anazoamini kuwa zitabamba zaidi na kutokea kufunika nyingine zitakazozikuta.


Video ya kibao ‘Shirawadu’ iko jikoni na itatoka mwishoni mwa mwezi huu, ikiwa sambamba na kibao chake kingine kipya cha mduara. 

No comments: