Tangazo

September 26, 2011

TBL YAIMWAGIA VIFAA VYA 10,000,000/- 'WIKI YA USALAMA BARABARANI'

Mkurugenzi wa Uhusiano wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Steve Kilindo (kulia) akimkabidhi Kamanda wa Polisi  Kikosi cha Usalama Barabarani, Kamishna Msaidizi Mwandamizi, Mohamed Mpinga msaada wa fulana na kofia vyenye thamani ya sh. mil. 10 kwa ajili ya maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa Usalama itakayoadhimishwa mkoani Kagera kuanzia Oktoba 3-8, mwaka huu. Hafla hiyo ilifanyika Dar es Salaam juzi.

Kamanda wa Polisi wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Kamishna Msaidizi Mwandamizi, Mohamed Mpinga  (kushoto) akimshukuru Mkurugenzi wa Uhusiano wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Steve Kilindo  baada ya kupatiwa na TBL msaada wa fulana na kofia vyenye thamani ya sh. mil. 10 kwa ajili ya maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa Usalama yatakayofanyika mkoani Kagera kuanzia Oktoba 3-8, mwaka huu. Hafla hiyo ilifanyika Dar es Salaam juzi.

Ofisa Uhusiano wa TBL, Dorris Malulu (kushoto) akiwa na Kamanda Mpinga (katikati) pamoja na Ofisa Usalama Barabarani.

 Meneja Miradi Maalum wa TBL, Emma Orio (kulia), akibadilishana mawazo na Ofisa Usalama Barabarani, wakati wa hafla hiyo.

No comments: