Tangazo

January 24, 2012

TAMASHA NAMBA MOJA AFRIKA MASHARIKI LAKARIBIA

Toleo la tisa la tamasha la Sauti za Busara litakalofanyika hapa Zanzibar kuanzia tarehe 8 mpaka 12 Februari 2012.
Baada ya kupokea zaidi ya maombi 600 ya wasanii waliotaka kushiriki kutoka nchi tofauti zaidi ya sitini, kati ya vikundi 31 vilichaguliwa kushiriki katika tamasha katika jukwaa kuu ndani ya Ngome Kongwe.

Miaka iliyopita baadhi ya wasanii waliowahi kushiriki ni kama:
Samba Mapangala & Orchestra Virunga (DRC/ Kenya), Bi Kidude (Tanzania), Thandiswa (Afrika Kusini), Bassekou Kouyate (Mali) na Didier Awadi (Senegal). Wasanii watakaoshiriki mwaka huu 2012 ni kama wafuatao,

Zanzibar: Kidumbaki JKU, Shirikisho Sanaa, Skuli ya Kiongoni, Swahili Vibes Band, Tandaa Traditional Group, Tausi Women's Taarab, Utamaduni JKU, Kidumbaki JKU, Wanafunzi wa SOS.
 
Zanzibar ( Pemba): Juhudi Taarab, Mkota Spirit Dancers.
 
Tanzania mainland: Lady Jaydee, Leo Mkanyia, Lumumba Theatre Group, Seven Survivor, Tunaweza Band, Jembe Culture Group, Jagwa Music , FM Academia.
 
Uganda: Ndere Troupe, Qwela.
 
Kenya: Ogoya Nengo, Super Mazembe.
 
Congo Brazzaville : Freddy Massamba.
 
South Africa: Tumi & The Volume.
 
Nigeria: Nneka.
 
Cape Verde: Ary Morais.
 
Comoros: Chébli Msaïdie.
 
Madagascar: Hanitra.
 
Reunion: Kozman Ti Dalon.
 
Sudan :Camirata Group.

Siku ya ufunguzi wa tamasha utajumuishwa na beni brass band, wapiga ngoma, wanawake wa mwanandege wanaotembea na miamvuli, Ngongoti, capoeira, na sarakasi.

 Maandamano haya yatazunguka Kisiwa na kuishia Ngome kongwe ambapo onyesho rasmi litaanza kupitia jukwaa kuu. Hii itakuwa ni siku nne mfululizo live muziki asilimia mia wa kiafrika ambao unatangaza Afrika na kukuza uchumi na fani ya muziki, pia tutaonyesha filamu za muziki wa Kiafrika , Nyongeza za Busara ni matukio mbali mbali yatakayo fanyika wakati wa tamasha.

Kuhusu tamasha la muziki la Sauti za Busara

Sauti za Busara sasa ni toleo lake la tisa linalotoa nafasi kwa ajili ya wanamuziki wa ndani kujifunza na kupata uzoefu kutoka sehemu mbalimbali duniani kote, hii ikiwa ni pamoja na kulitambulisha tamasha la Afrika mashariki kwa wageni.Katika jamii yoyote ni muhimu kwa afya na maendeleo ya mitindo ya muziki.

Sauti za Busara ni mfano wa tukio liloundwa na kuendeleza muziki, hii ikiwa ni pamoja kwa wenyeji na wageni kwa thamani ya kipekee, utajiri na utofauti wa muziki kutoka katika kila kanda. Inaonyesha kuwa kuna vivutio katika muziki wetu wa jadi , pamoja na ajira na kipato kinachopatikana kuendeleza hili.

Kisanii, warsha na semina za kiufundi kuwa sehemu muhimu ya shughuli za Busara, yenye lengo kwa wanamuziki, wataalamu wa vyombo vya habari, mameneja wa sanaa, mafundi na wafanyakazi wa kitamaduni kutoka kanda. Warsha hizi zimesaidia kujenga maarifa na ujuzi kwa manufaa ya muda mrefu ya utamaduni wa Afrika Mashariki.

Kwa maelezo zaidi
Maelezo ya Wasanii Ratiba la Tamasha Kuhoji Wasanii

Kwa mahojiano na maswali zaidi tafadhali wasiliana nasi kupitia press@busara.or.tz

Wadhamini
Sauti za Busara 2012 imedhaminiwa na: The Norwegian Embassy, HIVOS, Mimeta, Roskilde Festival Charity Society, Grand Malt, Toyota, Commercial Bank of Africa, Goethe Institut, African Leisure Centre, fly540, Memories, SMOLE II, Zanlink, Azam Marine, Embassy of France, Maru Maru Hotel, Zanzibar Grand Palace Hotel, fRoots, Times FM, Multi-Color Printers, Ultimate Security,Tabasam Tours, Emerson Spice, Monsoon Restaurant, Southern Sun Dar es Salaam, Mercury's, Archipelago Restaurant, Stone Town Café, www.zanzibar.net

Kwa picha  za tamasha
www.busaramusic.org/SzB2011pics  www.busaramusic.org/SzB2010pics
* Ukitaka picha za kuchapisha wasiliana nasi


No comments: