Tangazo

March 29, 2012

Joaquine De-Mello atunukiwa Tuzo ya Mwanamke Jasiri Tanzania 2012

Ofisa wa Mambo ya Nje wa Ubalozi wa Marekani nchini Tanzania, Dana Banks akizungumza wakati wa hafla ya kumtunuku Tuzo ya Mwanamke Jasiri Tanzania 2012, Bi. Joaquine De-Mello iliyofanyika katika ubalozi huo jijini Dar es Salaam leo Machi 29.12. De-Mello ni Mwanasheria Kitaaluma na amekuwa Kamishna wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora tangu Mwaka 2008. Aidha Ubalozi wa Marekani hapa Nchini umeamua kumtunuku tuzo hiyo kutokana na juhudi zake za kutetea Haki za Wanawake hapa nchini. PICHA ZOTE/JOHN BADI

Sehemu ya wageni waalikwa waliohudhuria hafla hiyo.

Kaimu Balozi wa Marekani hapa nchini, Robert Scott  akisoma hotuba kabla ya kukabidhi tuzo hiyo.

Sehemu ya wageni waalikwa waliohudhuria hafla hiyo.

Wimbo wa taifa wa Tanzania na Marekani ulipigwa na Kwaya ya Vijana ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzani la Kijitonyama (Haipo pichani).
Kaimu Balozi wa Marekani hapa nchini, Robert Scott akikabidhi Tuzo ya Mwanamke Jasiri Tanzania 2012, Bi. Joaquine De-Mello.

Mwanamke Jasiri Tanzania 2012, Bi. Joaquine De-Mello akitoa neno la shukrani baada ya kupokea tuzo.
Robert Scott akimpongeza De-Mello baada ya kutoa neno la shukrani.

Mwanzilishi na Mwenyekiti wa Alice Foundation ambaye pia ni Mkurugenzi wa Alice Fashion World, Alice James Dosi akikabidhi zawadi ya maua kwa De-Mello kama ishara ya kumpongeza.
Pongezi ziliendelea kumiminika.

De-Mello akiwa katika picha ya pamoja na Robert Scott na Dana Banks.
De-Mello akiwa katika picha ya pamoja na maofisa kutoka Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora. Wa (tatu kulia) ni Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji mstaafu Amir Manento.

De-Mello akiwa katika mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA) ambaye ni mmoja kati ya waliowahikupata tuzo kama hiyo Mwaka 2010, Bi. Ananilea Nkya (kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Under The Same Sun (UTSS) Tawi la Tanzania, Bi. Vicky Ntetema (kulia).

No comments: